1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOSCOW: Wanamgambo wauawa nchini Russia.

4 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCVD

MOSCOW

Wizara ya mambo ya ndani ya Russia imearifu kwamba maafisa wa usalama wamewaua wanamgambo wanne kwenye mji mmoja wa eneo la Ingushetia linalopakana na Chechnya.

Wakazi wengi wa eneo hilo ni wa kabila linalokaribiana na Wachechnya.

Msemaji wa wizara hiyo amesema watu hao waliuawa wakati wa mapigano ya risasi kwenye sehemu ya makazi.

Russia inaamini wanamgambo wanaounga mkono Chechnya kujitenga, wamejificha katika eneo hilo.