1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwaka mmoja wa rais Mohamoud Somalia

11 Septemba 2013

Baada ya mwaka wa kwanza madarakani kama rais wa taifa ambalo ni mahali pa hatari zaidi duniani na taifa lililoshindwa, Hassan Sheikh Mohamoud bado anapambana na uwezo mdogo wa kifedha, rushwa,

https://p.dw.com/p/19fb5
Residents walk past the campaign billboard of Somalia's presidential candidate Hassan Sheikh Mohamud in Somalia's capital Mogadishu, September 9, 2012. Somalia's lawmakers voted overwhelmingly on Monday for Mohamud as the country's next president, with the streets of the capital erupting into celebratory gunfire, Reuters witnesses said. Two of the four candidates who made it to the second round of voting opted out, leaving the incumbent President Sheikh Sharif Ahmed and Mohamud.Picture taken September 9, 2012. REUTERS/Feisal Omar (SOMALIA - Tags: POLITICS ELECTIONS)
Rais wa Somalia - Hassan Sheikh MohamudPicha: picture-alliance/dpa

Matatizo hayo ni pamoja na ukosefu wa utoaji huduma ,mauaji ya maafisa wa serikali nchini humo , ikiwa ni pamoja na jaribio dhidi ya maisha yake binafsi.

Rais wa Somalia , ambaye jana Jumanne Septemba 10 alisherehekea siku 365 tangu alipochaguliwa kuwa rais na wabunge, amekuwa na wakati mgumu sana katika mwaka wake wa kwanza wa kipindi chake cha miaka minne ya uongozi.

LONDON, UNITED KINGDOM - MAY 7: Prime Minister David Cameron (L) and Somali President Hassan Sheikh Mohamud (C) shake hands after making their opening speeches during the Somali conference, on May 7, 2013 in London, England. The international conference aims to help rebuild the east African country after more more than two decades of conflict. (Photo by Andrew Winning - WPA Pool/Getty Images)
rais Hassan Sheikh Mohamud(kati)na waziri mkuu wa Uingereza Cameron(kulia)Picha: Getty Images

Wadadisi wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa sio tu kwamba Mohamud analazimika kupambana na makundi ya wapiganaji wa Kiislamu kama al-Shabaab , kundi ambalo limefanya mashambulio kadha hivi karibuni ya kigaidi katika mji mkuu Mogadishu licha ya kufurushwa kutoka miji kadha muhimu katika taifa hilo la pembe ya Afrika , na ongezeko la idadi ya majimbo yanayotaka kujitenga, pia anakabiliwa na hali inayoongezeka ya kukata tamaa miongoni mwa Wasomali.

A picture taken on March 2, 2012 shows Ethiopian troops standing on an army tank at an air base in the city of Baido, which was taken over from Shebab rebels on February 22. Truckloads of Ethiopian and Somali troops on February 22 captured the strategic Somali city of Baidoa from Al-Qaeda-allied Shebab insurgents, who vowed to avenge their biggest loss in several months. Baidoa, 250 kilometres (155 miles) northwest of the capital Mogadishu, was the seat of Somalia's transitional parliament until the hardline Shebab captured it in 2009. Ethiopia says it is in the country to support Somalia?s transitional government to stamp out Shebab insurgents, but says it does not plan to remain in the country for the long term. AFP PHOTO / JENNY VAUGHAN (Photo credit should read JENNY VAUGHAN/AFP/Getty Images)
Jeshi la SomaliaPicha: JENNY VAUGHAN/AFP/Getty Images

Abdi Aynte , muasisi na mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya turathi kwa ajili ya mitaala ya sera, (HIPS), taasisi ya kwanza nchini humo ya kubadilishana maarifa, amesema kuwa Mohamud ameshindwa kuleta matunda katika mwaka wake wa kwanza.

Sera ya nguzo sita

"Sera ya nguzo sita ilikuwa ya kutia moyo, lakini utoaji wa huduma kwa umma haukuwapo kabisa," Aynte ameliambia shirika la habari la IPS mjini Nairobi. Sera ya nguzo sita ilikuwa mkakati wa Mohamud wa kuleta usalama , uthabiti, haki , ufufuaji wa uchumi, na kutoa huduma kwa Somalia.

"Kwa hiyo hakuna cha ajabu kwamba hatuna maendeleo yanayoonekana yaliyofikiwa kuelekea kutimiza hata moja kati ya nguvu hizo."

Residents use a donkey cart as they flee from fighting between Somalia government and Somalia's Al-Qaeda linked Shebab insurgents in southern Mogadishu, on October 12, 2011. African peacekeepers and Somali government forces flushed Islamist rebels out of one of the few pockets of the capital Mogadishu still under militant control, a spokesman for the Amisom said. AFP PHOTO/Mahamed Abdiwahab (Photo credit should read Mahamed Abdiwahab/AFP/Getty Images)
Wasomali wamekimbia makaazi yao baada ya ghasiaPicha: Mohamed Abdiwahab/AFP/Getty Images

Wasomali wameishi kwa karibu miaka 20 katika vita , umasikini na kutawanyika kufuatia kuondolewa madarakani dikteta na rais wa zamani Mohamed Siad Barre mwaka 1991. Nchi hiyo haijakuwa na serikali kuu hadi mwaka 2000, baada ya kuwa na serikali kadha za mpito ambazo zilichaguliwa.

Pia kuna huduma muhimu chache ama vituo vya huduma za afya vichache nchini humo , huduma nyingi hata hivyo zikitolewa na mashirika yasiyo ya kiserikali. Kwa muda wa miaka 20 shirika la madaktari wasio na mipaka , Medecins Sans Frontieres, lilikuwa moja kati ya watoaji wachache wa huduma ya afya ya msingi nchini Somalia.

Lakini mwezi Agosti shirika hilo lilijitoa kutoka nchini humo baada ya kuuwawa na kusumbuliwa kwa wafanyakazi wake kila mara na kufanya kuwa vigumu kwa shirika hilo kufanyakazi nchini humo.

Lakini wasaidizi wa Mohamud wamekuwa wepesi kumtetea profesa huyo wa zamani na mwanaharakati wa vyama vya kijamii, ambaye alinusurika katika jaribio la kuuawa wakati akisafiri kwenda katika mji wa kusini nchini humo wa Merca hapo Septemba 3.

Matatizo ya kifedha

Msemaji wa rais Abdirahman Omar Osman ameliambia shirika la habari la IPS kuwa nchi hiyo ina matatizo makubwa ya kifedha ambayo yanafanya kuwa vigumu kwa Mohamud kuweza kutimiza ahadi zake.

"Serikali haina fedha za kutosha kufanya kila kitu," Osman ameliambia shirika hilo la IPS mjini Mogadishu.

ARCHIV - Die zweijährige Tsclaha, die nur sechs Kilogramm wiegt, isst am 24.07.2005 in einem Ernährungszentrum im nigerianischen Maradi im Rahmen einer Therapie einen Mehlbrei. Nach der verheerenden Dürrekatastrophe in Somalia und Kenia im vergangenen Jahr bahnt sich in Afrika ein neues Hungerdrama an. Betroffen ist der Westen der Sahelzone. Allein in Niger und Mauretanien litten bereits sechs Millionen Menschen Hunger, und auch in Mali und im Tschad sei die Lage bedrohlich, sagte Ralf Südhoff, Leiter des Berliner Büros des Welternährungsprogramms (WFP), der Nachrichtenagentur dpa. EPA/STR (zu dpa 0260 am 27.01.2012) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Njaa na magonjwa nchini SomaliaPicha: picture-alliance/dpa

"Mapato ya serikali ya kila mwezi ni wastani wa dola milioni tatu kutokana na bandari ya Mogadishu na uwanja wa ndege, wakati huo huo bajeti inayohitajika kutekeleza shughuli za kawaida za kila siku ni kiasi cha dola milioni 20 kila mwezi," amesema.

Hata hivyo, tarakimu zilizotolewa na Osman zinapingana na zile alizotoa naibu mkurugenzi mkuu wa bandari ya Mogadishu Abdiqani Osman Kabareto. Kabareto ameimbia redio moja nchini humo ya Ergo mwezi August kuwa bandari ya mjini Mogadishu inauwezo wa kuzalisha kiasi cha kati ya dola milioni nne na tano kila mwezi.

"Fikiria serikali ikiwa na uhaba wa aina hiyo wa bajeti ikijaribu kujenga na kuunda taasisi kutoka mwanzo kabisa . Hapa ndio penye tatizo. Sio kwamba serikali haiko tayari, ni matatizo ya upungufu wa fedha," amesema Osman.

Mohammed Ali , mhitimu wa chuo kikuu cha Somad , ambacho Mohamud alisaidia kukiasisi, ameliambia shirika hilo la IPS kuwa licha ya kuwa aliunga mkono kuchaguliwa kwa Mohamud , anahisi kuwa hakuna cha kufurahia baada ya mwaka mmoja madarakani.

Mwandishi: Sekione Kitojo / IPS

Mhariri : Mohammed Abdul Rahman