1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwenyekiti mpya wa Ukanda wa sarafu ya Euro

Abdu Said Mtullya22 Januari 2013

Mawaziri wa fedha wa nchi zinazotumia sarafu ya Euro wamemchagua Jeroen Dijsselbloem kutoka Uholanzi kuwa Mwenyekiti mpya wa jumuiya yao.

https://p.dw.com/p/17Ong
Aliyekuwa Mwenyekiti wa kundi la sarafu ya Euro Waziri Mkuu wa Luxembourg Jean-Claude Juncker na Mwenyekiti mpya Jeroen Dijsselbloem wa Uholanzi.
Aliekuwa Mwenyekiti wa kundi la sarafu ya Euro,Waziri Mkuu wa Luxembourg Jean Claude Juncker na Mwenyekiti mpya Jeroen Dijsselbloem wa UholanziPicha: Reuters

Mholanzi huyo anaechukua nafasi iliyoachwa wazi na Jean Claude Juncker  alipingwa na Uhispania tu. Mwenyeketi huyo mpya Dijssebloem ameshaanza kazi  yake licha ya upinzani wa Uhispania.

Mwenyekiti wa hapo awali Jean Claude Juncker aliwaambia waandishi wa habari  mjini Burssels kwamba mawaziri wa fedha wa nchi za ukanda wa sarafu ya  Euro wamemteua Dijsselbloem kuwa mwenyekiti wao. Uteuzi huo umekuja wakati wa kufaa kwa bwana Juncker alieuliza kwa mzaha jee nani atakuja kuniondoa mahala hapa? 

Dijsselbloem atautumikia wadhifa wake mpya kwa muda wa miezi 30 lakini wakati huo huo ataendelea kuwa Waziri wa fedha wa nchi yake Uholanzi.

Mwenyekiti mpya ametoa mwito wa kufanya kazi zaidi ili kuudumisha mfumo wa kiuchumi na kijamii wa barani Ulaya unaothinimiwa sana. Amesema Ili kuweza  kuudumisha mfumo huo inapasa kufanya kazi ili kuleta ustawi na kutenga nafasi  mpya za ajira na wakati huo huo  kuziweka bajeti sawa.Amesema malengo hayo  yanaungwa mkono na mawaziri wa fedha wote wa jumuiya ya sarafu ya Euro.

 Mwenyekiti mpya tayari atapigwa darubini kwenye mazungumzo ya mawaziri wa fedha kutoka nchi zote 27 za Umoja  wa Ulaya mjini Brussels ambapo mawaziri  hao watalijadili pendekezo la nchi 11 za ukanda wa Euro juu  ya kuanzisha utaratibu  wa kuzitoza kodi shughuli zote za kifedha.

Mwenyekiti mpya,Dijsselbloem wa kundi la nchi zinazotumia safaru ya Euro amesema kwake ni heshima kubwa kuchaguliwa kushika nafasi iliyoachwa wazi na Jean Claude Juncker. Dijsselbloem mwenye umri wa miaka 46 anachukua nafasi  hiyo wakati ambapo nchi za kusini mwa Ulaya zimelemewa na mzigo wa madeni.

 Waziri wa fedha wa Ufaransa Pierre Moscovici amesema anatummai kwamba Mwenyekiti mpya Jeroen Dijsselbloem ataleta urari katika jumuiya hiyo. Lakini hadi wiki iliyopita Ufaransa ilikuwa na mashaka juu ya mwenyekiti huyo mpya.Hatahivyo Waziri wa fedha  wa Ufaransa  Moscovici aliimpigia  kura mholanzi  huyo.

Waziri  wa  fedha  wa a Ujerumani  Wolfgang Schäuble amesema uteuzi wa Dijsselbloem ni jambo  zuri  wakati rais   wa  Baraza  la Umoja  wa a Ulaya Hermann Van  Rompuy amesema  viongozi   wa  nchi  zote  17  za ukanda   wa  sarrafu  ya   Euro  wanamuunga mkono. Hermann  Van  Rompuy amesema ana uhakika   kwamba  Dijsselbloem ndiye anaefaa.

Mwandishi:Hasselbach  Christoph.

Tafsiri:Mtullya  Abdu.

Mhariri:Josephat Charo