1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mzozo baina ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Rwanda

22 Juni 2012

Mzozo kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda unaonekana kuchukua sura mpya.

https://p.dw.com/p/15JbD
Mji wa Goma walikokamatwa raia wa Rwanda
Mji wa Goma walikokamatwa raia wa RwandaPicha: AP

Siku mbili baada ya raia 11 wa Rwanda kukamatwa mjini Goma katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na kupigwa vibaya kisha kuvukishwa mpaka kwa nguvu hadi Rwanda, nchi hiyo imeionya kwa barua Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Rwanda Bi Louise Mushikiwabo amesema kuendelea kuitaja Rwanda kama chanzo cha tatizo la DRC ni hatari kwa raia wake na raia wenye asili ya Rwanda waishio DRC.

Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi.

(Kusikiliza ripoti hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)

Mwandishi: Sylvanus Karemera

Mhariri: Josephat Charo