1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mzozo wa Euro unahatarisha uchumi duniani

20 Septemba 2011

Italia imepata pigo baada ya shirika la Marekani la Standard & Poors linalotathmini iwapo serikali zinaaminiwa kupewa mikopo, kuamua kushusha kiwango cha uwezo wa Italia kuyalipa madeni yake.

https://p.dw.com/p/RmjT
ARCHIV - Der griechische Finanzminister Evangelos Venizelos und EZB-Präsident Jean-Claude Trichet (l) unterhalten sich am 12.07.2011 in Brüssel. Am Montag (19.09.) werden Venizelos mit der «Troika» - den Geldgebern von EU, Internationalem Währungsfonds (IWF) und Europäischer Zentralbank (EZB) in einer Telefonkonferenz sprechen. Foto: Olivier Hoslet dpa (zu dpa 0380 vom 19.09.2011) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Waziri wa Fedha wa Ugiriki, Evangelos Venizelos(kulia) na Rais wa Benki Kuu ya Umoja wa Ulaya, Jean-Claude TrichetPicha: picture-alliance/dpa

Wakati huo huo, Ugiriki inayokabiliwa na kitisho cha kufilisika, inajitahidi kama iwezavyo, kupata msaada wa dharura kutoka kwa Umoja wa Ulaya na Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF. Waziri wa Fedha wa Ugiriki, Evangelos Venizelos ameashiria kuwa serikali yake ipo tayari kuchukua hatua kali zaidi za kubana matumizi na kupunguza nakisi katika bajeti. Mkutano uliofanywa kwa njia ya simu, jana usiku, kati ya waziri huyo wa fedha na wataalamu wa kiuchumi wa Umoja wa Ulaya, Benki Kuu ya Ulaya na Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF, ulimalizika haraka bila ya mafanikio makubwa kupatikana.Hata hivyo, Venizelos amesema, majadiliano hayo yalikuwa na manufaa na umuhimu. Kwa mujibu wa wizara ya fedha ya Ugiriki na Halmashauri ya Umoja wa Ulaya, majadiliano hayo yataendelea leo jioni kwa njia ya simu.

(FILE) A bus drives past the International Monetary Fund (IMF) building in Washington, DC, 02 August 2004. Financial institutions could suffer losses as high as 945 billion dollars from the ongoing credit crisis and should take immediate action to increase transparency and correct excessive risk strategies that sparked the current turmoil, the International Monetary Fund said 08 April 2008. The Washington-based lender said losses from already falling0 housing prices and the resulting subprime mortgage market crisis would total 565 billion dollars. EPA/MATTHEW CAVANAUGH +++(c) dpa - Report+++
Makao makuu ya IMF, mjini Washington,MarekaniPicha: DPA

Hapo awali, mwakilishi wa IMF nchini Ugiriki, Bob Traa alifafanua hatua zinazopaswa kuchukuliwa na serikali ya Ugiriki ili kuweza kupata mkopo wa Euro bilioni 8 unaohitajiwa kwa dharura na nchi hiyo. Alieleza:

"Kwa maoni yetu, kodi ya pato isiendelee kupandishwa. Kwani hiyo ni hatua isiyoweza kuendelezwa kiuchumi wala kisiasa."

Anasema, kwanza serikali ya Ugiriki inapaswa kurekebisha mfumo wa kutoza kodi, kwani mpaka sasa haukuleta matokeo yaliyotazamiwa. Vile vile ichukue hatua kali kupambana na tatizo kubwa la wakwepa kodi.Ripoti nzuri kutoka kwa wataalamu hao ndio itakayosaidia kuamua, iwapo Ugiriki ipewe kitita hicho cha Euro bilioni 8 kutoka msaada wa fedha wa Euro bilioni 110 uliokubaliwa hapo awali. Taarifa rasmi kutoka Athens zinasema, ikiwa Ugiriki haitopewa fungu hilo la fedha, basi serikali inakabiliwa na kitisho cha kufilisika mwezi wa Oktoba.

epa02773071 Italian Prime Minister Silvio Berlusconi speaks at a press conference after the Council of Ministers meeting in Rome, Italy, 09 June 2011. EPA/MAURIZIO BRAMBATTI +++(c) dpa - Bildfunk+++
Waziri Mkuu wa Italia, Silvio BerlusconiPicha: picture-alliance/dpa

Kwa upande mwingine, Italia nayo leo imepata pigo, baada ya shirika la Standard & Poor´s kushusha kiwango cha uwezo wa nchi hiyo kulipa madeni yake. Hatua hiyo imeshtusha na imesababisha thamani ya Euro kuanguka katika masoko ya fedha asubuhi ya leo. Vile vile inazidisha wasiwasi katika kanda inayotumia sarafu ya Euro. Wachambuzi wanasema, hatua hiyo itaathiri uchumi duniani kwa hivyo viongozi hawana budi kuwa na msimamo mmoja na kuchukua hatua imara kuutenzua mzozo wa madeni katika kanda ya Euro. Kwa maoni ya wataalamu wa kiuchumi, mzozo huo wa fedha unapaswa pia kushughulikiwa kwa dharura katika mikutano ya IMF, Benki ya Dunia na kundi la G20 linalojumuisha nchi tajiri zilizoendelea kiviwanda na zinazoinukia kiuchumi duniani, inayofanywa wiki hii mjini Washington, Marekani.

Mwandishi:Martin,Prema

Mhariri: Josephat Charo