1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NAIROBI: Wafanyakazi wa Umoja wa mataifa waondoka kutoka Somalia

13 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD3J

Umoja wa mataifa umewaondoa wafanyakazi wake kwa muda kutoka Somalia kufuatia vitisho vya kuuawa. Maafisa wa Umoja wa mataifa mjini Nairobi nchini Kenya, hawakusema ni nani ametoa vitisho hivyo lakini wamesema wanavizingatia kwa makini. Wapiganaji wa muungano wa makundi ya waislamu sasa wanalidhibiti eneo la kusini mwa Somalia ukiwemo mji mkuu Mogadishu na serikali ya mpito ya rais Abdullahi Yussufu inaonekana kuwa dhaifu kuweza kudhibiti hali ya mambo Somalia.