1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NAIROBI:Viongozi wa ODM wadokeza mfumo wa kumteuwa mgombea wa urais

22 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBWy

Viongozi wa kundi la Orange Democratic Movement nchini Kenya bado wanajadiliana kuhusu nani atakae kuwa mgombea wa urais wa chama hicho katika uchaguzi ujao wa Desemba.

Viongozi hao wamedokeza kwamba watafikia uamuzi huo mwezi Septemba katika mkutano wao mkubwa utakao fanyika katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi.

Rais Kibaki huenda akakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwenye chama hicho.