1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ndoto ya Cote D'Ivoire yaota mbawa

4 Februari 2013

Nigeria na Burkina Faso zakamilisha orodha ya timu nne zilizoingia katika nusu fainali ya kombe la mataifa ya Afrika huko Afrika kusini.Borussia Dortmund yanyakua nafasi ya pili ligi ya Ujerumani Bundesliga.

https://p.dw.com/p/17XqP
RUSTENBURG, SOUTH AFRICA - FEBRUARY 03: Ogenyi Onazi of Nigeria and Didier Drogba of Ivory Coast compete during the 2013 Orange African Cup of Nations 3rd Quarter Final match between Ivory Coast and Nigeria, at Royal Bafokeng Stadium on February 03, 2013 in Rustenburg, South Africa. (Photo by Lefty Shivambu/Gallo Images/Getty Images)
Ni pambano baina ya Cote D'Ivoire na NigeriaPicha: Getty Images Europe

Burkina Faso na Nigeria zimekamilisha orodha ya timu nne zilizosalia katika kinyang'anyiro cha kuwania ubingwa wa mataifa ya Afrika , AFCON 2013 nchini Afrika kusini jana(03.02.2013) wakati Cote D'Ivoire ambayo ilikuwa inapigiwa upatu kutoroka na taji la mwaka huu la kombe la Afrika ikishindwa kutimiza matarajio hayo.

RUSTENBURG, SOUTH AFRICA - FEBRUARY 03: Gervinho of Ivory Coast and Brown Ideye of Nigeria vie for the ball during the 2013 Orange African Cup of Nations 3rd Quarter Final match between Ivory Coast and Nigeria, at Royal Bafokeng Stadium on February 03, 2013 in Rustenburg, South Africa. (Photo by Lefty Shivambu/Gallo Images/Getty Images)
Gervinho wa Cote D'Ivoire akipambana na Brown Ideye wa NigeriaPicha: Getty Images Europe

Burkina Faso iliishinda Togo kwa bao 1-0 baada ya mchezo kuingia katika dakika za nyongeza na Jonathan Pitroipa aliipatia ushindi timu yake katika uwanja wa Nelspruit ambapo kabla ya hapo Nigeria ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tembo wa Cote D'Ivoire katika uwanja wa Rustenburg na kuweka mashindano haya wazi kwa yoyote kwa hivi sasa.

Nusu fainali

Nigeria sasa itapambana na Mali katika nusu fainali mjini Durban siku ya Jumatano na Ghana itakwaana na Burkina Faso uwanjani Nelspruit siku hiyo hiyo, michezo itakayoamua ni timu gani mbili zitaingia katika fainali ya mwaka huu kuwania ubingwa wa mataifa ya Afrika.

Nigeria walipewa nafasi ya asilimia 20 tu ya ushindi na kocha wao Stephen Keshi katika uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace. Lakini bao la Sunday Mba , dakika 12 kabla mpira kumalizika liliendeleza mfululizo wa ndoto za jinamizi kwa Didier Drogba na kikosi kizima cha Tembo wa Cote D'Ivoire ambao walipigiwa upatu kushinda ubingwa wa Afrika mara tano lakini mara zote wamekaribia tu kufanya hivyo.

Ni sababu gani inasosababisha ndoto ya Drogba na kikosi cha Cote D'Ivoire mara nyingi kuota mbawa? Swali hili nilimuuliza Mtemi Ramadhani mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania na pia afisa wa zamani wa shirikisho la kandanda la Tanzania TFF, ambaye amerejea hivi karibuni mjini Dar Es Salaam kutoka Afrika kusini ambako alikuwa akihudhuria michezo hii ya kombe la mataifa ya Afrika. Sikiliza mahojiano na Mtemi Ramadhani hapo chini.

Kusikiliza mahojiano na Mtemi Ramadhani bonyeza alama za spika hapo chini:

Didier Drogba na kizazi kinachoitwa cha dhahabu cha wachezaji wa Cote D'Ivoire walitoka uwanjani jana wakiwa vichwa chini baada ya kushindwa kwa mara nyingine tena kutimiza matarajio ya wengi kuwa wanaweza kuvishwa taji la wafalme wa soka katika bara la Afrika msimu huu.

Ndoto yaota mbawa

Kwa Drogba , ambaye anatimiza umri wa miaka 35 mwezi ujao, hii ilikuwa fursa yake ya mwisho ya kulinyakua taji hili la mataifa ya Afrika.

epa03092182 Didier Drogba of Ivory Coast reacts after scoring the first goal of the match during the Africa Cup of Nations Quarterfinal match between Ivory Coast and Equatorial Guinea in Malabo, Equatorial Guinea, 04 February 2012. EPA/STR EDITORIAL USE ONLY +++(c) dpa - Bildfunk+++
Didier DrogbaPicha: picture-alliance/dpa

Wachezaji wengine katika kikosi hicho kilichopewa nafasi kubwa lakini kimeshindwa kupata mataji kama Kolo Toure mwenye umri wa miaka 31, Didier Zokora mwenye umri wa miaka 32 na mlinda mlango Boubacar Barry mwenye umri wa miaka 33 , pia nao watakuwa na hisia kama Drogba za kujihisi hawana chao.

Jopo la wataalamu wa shirikisho la kandanda duniani FIFA litaangalia uwezekano wa kubadilisha namna sheria ya kuotea mpirani ,"offside", inavyotafsiriwa wakati wa mkutano mkuu wa shirikisho hilo mwezi ujao. Pia FIFA inasema kuwa jopo lake hilo pia litaangalia njia ya kuziba mwanya kuhusiana na mpira wa kuanzishwa na refa kwa kudondoshwa baada ya mpira kusimama kwa muda uwanjani, baada ya Shakhtar Donetsk kufunga goli la kutatanisha dhidi ya Nordsjaelland katika Champions League msimu huu.

Matapeli wa kupanga matokeo

Wakati huo huo polisi katika bara la Ulaya wameonya leo kuwa hadhi ya mchezo wa mpira wa miguu iko katika wakati mgumu baada ya kufichua kuwa wamevunja mtandao wa kihalifu wa kupanga matokeo ya michezo kadha , ikiwa ni pamoja na Champions League na michezo ya kombe la dunia.

Polisi ya Ulaya Europol imesema kuwa uchunguzi uliofanywa katika nchi tano umegundua shaka katika michezo 380 iliyoathirika kutokana na kampuni la kuweka dau na kuagulia nani mshindi, ambalo shughuli zake ambazo ni kinyume na sheria zimesambaa hadi kwa wachezaji, waamuzi na maafisa duniani kote katika viwango vyote vya mchezo huo.

Ligi za Ulaya :

Bundesliga ilikamilisha mchezo wake wa 20 jana Jumapili, ambapo mabingwa watetezi Borussia Dortmund iliponyakua nafasi ya pili katika msimamo wa ligi , baada ya mpambano mkali wa vuta nikuvute dhidi ya Bayer Leverkusen. Borussia Dortmund ilipata ushindi wa mabao 3-2. Kocha wa mabingwa hao watetezi Borussia Dortmund , Jürgen Klopp amesema kuwa huo ulikuwa mchezo mgumu sana kwa mabingwa hao.

Fußball Bundesliga 20. Spieltag: Bayer Leverkusen - Borussia Dortmund am 03.02.2013 in der BayArena in Leverkusen (Nordrhein-Westfalen). Dortmunds Robert Lewandowski, Marco Reus, Jakub Blaszczykowski, Mario Götze, Nuri Sahin und Marcel Schmelzer jubeln über das 0:1 durch Reus. Foto: Bernd Thissen/dpa (Achtung Hinweis zur Bildnutzung! Die DFL erlaubt die Weiterverwertung von maximal 15 Fotos (keine Sequenzbilder und keine videoähnlichen Fotostrecken) während des Spiels (einschließlich Halbzeit) aus dem Stadion und/oder vom Spiel im Internet und in Online-Medien. Uneingeschränkt gestattet ist die Weiterleitung digitalisierter Aufnahmen bereits während des Spiels ausschließlich zur internen redaktionellen Bearbeitung (z. B. via Bilddatenbanken).) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Borussia Dortmund wakishangiria bao dhidi ya LeverkusenPicha: picture alliance / dpa

Bayern Munich inayoongoza ligi hiyo, ina points 51 kibindoni , ilipata ushindi wa uhakika wa mabao 3-0 dhidi ya Mainz 05 siku ya Jumamosi.

Borussia Dortmund inashikilia nafasi ya pili sasa ikiwa na points 39. Bayer Leverkusen imeteremka hadi nafasi ya tatu ambapo ina points 37.

Premier League

Manchester United iliongeza mwanya wa points kileleni mwa msimamo wa ligi ya Uingereza Premier League hadi points tisa baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Fulham na Manchester City ikatoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Liverpool jana Jumapili.

City watamshukuru zaidi mshambuliaji wao Sergio Kun Aguero baada ya kufunga bao zuri ajabu kwa kuuzungusha mpira akiwa katika kibendera cha kona hadi wavuni, na kuipatia timu yake sare muhimu katika wakati ambao City ilionekana kudoda.

Goli alilojifunga mwenyewe Cristiano Ronaldo lilitosha kuwaadhibu mabingwa watetezi wa ligi ya Uhispania La Liga, Real Madrid na kupata kipigo kingine cha bao 1-0 dhidi ya Granada, na kuongeza athari zaidi katika kampeni yao ya kutetea ubingwa wao. Lionel Messi alipachika bao la 12 katika michezo 12 aliyocheza na kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Valencia.

Portugal's Cristiano Ronaldo reacts during the Euro 2012 semi-final soccer match against Spain at Donbass Arena in Donetsk, June 27, 2012. REUTERS/Charles Platiau (UKRAINE - Tags: SPORT SOCCER)
Cristiano Ronaldo wa Real MadridPicha: Reuters

Super Mario

Mario Balotelli alipachika mabao mara mbili katika ushindi wa AC Milan mwanzoni mwa mshambuliaji huyo kuichezea timu aliyoishabikia tangu utotoni mwake na kuipa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Udinese. Milan imesogea hadi katika nafasi ya nne ikiwa na pints 40 ikitanguliwa na majirani zao wa Inter kwa tofauti ya magoli. Viongozi wa ligi hiyo Juventus Turin inaongoza kwa points tatu mbele ya SSC Napoli wakati timu zote hizo zilipata ushindi dhidi ya Chievo Verona na Catania.

FILE - Italian forward Mario Balotelli celebrates after scoring the 0-2 during the UEFA EURO 2012 semi-final soccer match Germany vs. Italy at the National Stadium in Warsaw, Poland, 28 June 2012. Photo: Marcus Brandt dpa (Please refer to chapters 7 and 8 of http://dpaq.de/Ziovh for UEFA Euro 2012 Terms & Conditions) (zu dpa:"Die italienische Mannschaft im Kurzporträt" vom 30.06.2012) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Super Mario BalotelliPicha: picture-alliance/dpa

Tennis:

Uhispania ambayo iko katika nafasi ya juu katika mchezo wa tennis duniani imeondolewa katika duru ya kwanza ya mashindano ya kombe la Davis kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2006 wakati Milos Raonic alipomshinda Guillermo Garcia-Lopez na kuipa Canada ushindi wa michezo 3-1 katika kundi lao jana Jumapili. Uhispania ambayo ni mabingwa wa kombe hilo mara tano ,ilionekana kupata taabu tangu mwanzo wa pambano hilo mjini Vancouver Canada na Raonic alizika ndoto zao kwa kumshinda Garcia Lopez kwa seti tatu kwa sifuri , 6-3 6-4 na 6-2.

Kwa taarifa hizo mpenzi msikilizaji ndio sina budi kusema tumefikia mwisho wa kuwaletea habari hizi za michezo kwa leo. Jina langu ni Sekione Kitojo, hadi mara nyingine kwaherini.

Mwandishi : Sekione Kitojo / rtre / afpe /

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman