1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW DELHI: Mafuriko yameathiri mamilioni kusini mwa Asia

5 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBbu

Mafuriko yaliyosababishwa na pepo za msimu wa mvua kubwa,yameathiri mamilioni ya watu kusini mwa bara la Asia.Takriban watu milioni 10 wamepoteza makazi yao.Mashirika yanayoshughulikia maafa hayo yamesema,maeneo yaliyoathirika vibaya zaidi ni Kaskazini ya India,Bangladesh na Nepal. Maafisa serikalini wamesema,nchini India peke yake,idadi ya watu waliopoteza maisha katika mafuriko hayo,imefikia 1,100.