1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK: Mwito kulaani mashambulizi ya Israel

25 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CByW

Wanadiplomasia wa Kipalestina wametoa mwito kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulaani mashambulizi ya angani yanayofanywa na Israel katika Ukanda wa Gaza na kukamatwa kwa zaidi ya wanachama 33 wa Hamas wa ngazi ya juu.Waziri wa elimu Nasseredine al-Shaer,wabunge § na wameya 4 ni miongoni mwa wanachama waliokamatwa,baada ya Ukingo wa Magharibi kuvamiwa na wanajeshi wa Israel.