1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK:Bhuto ataka kurejea Pakistan

1 Aprili 2007
https://p.dw.com/p/CCDe

Aliyekuwa waziri Mkuu wa Pakistan bibi Benazir Bhuto amesema anakusudia kurejea nchini humo mwaka huu licha ya uwezekano kwamba anaweza kutiwa ndani.

Bibi Bhuto amesema itakuwa heshima kwake ikiwa atachaguliwa tena kuwa waziri mkuu.Waziri Mkuu huyo wa zamani amewaambia waandishi habari mjini New York kuwa hafikiri kuwa anaweza kukamatwa.