1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK:Kansela Merkel ahimiza juhudi za kupambana na ongezeko la joto

25 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBMm

Kansela wa Ujerumani bibi Angela Merkel ametoa mwito juu ya kupambana na ongezeko la joto duniani. Akizungumza mjini New York kwenye mkutano uliodhaminiwa na Umoja wa Mataifa juu ya suala la hali ya hewa Kansela Merkel amezitaka nchi za viwanda ziwe mstari wa mbele katika juhudi za kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa.