1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NICOSIA.Watu kumi na wawili waokolewa na kikosi cha wanamaji cha Ujerumani

24 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CCzo

Kikosi cha jeshi la wanamaji cha Ujerumani kimewaokowa mabaharia 12 wa meli ya Syria iliyoshika moto katika eneo la mashariki la bahari ya Mediterranean.

Jeshi la Ujerumani linalotekeleza mpango wa amani wa umoja wa mataifa katika pwani ya Lebanon liliwapeleka kwa helikopta mabaharia wawili katika hospitali ya kisiwa cha Cyprus na kuwaokowa mabaharia kumi 10 waliosalia.