1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nigeria kuimarisha usalama wa safari za ndege

Josephat Nyiro Charo4 Juni 2012

Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan hii leo (04.06.2012) ameahidi kuchukua hatua madhubuti kuimarisha usalama wa usafiri wa ndege nchini humo kufuatia ajali ya ndege hapo jana ambapo zaidi ya watu 150 waliuwawa.

https://p.dw.com/p/157ok
The wreckage of a plane burns in Nigeria's commercial capital Lagos, June 3, 2012. A plane that crashed into a downtown area of the Nigerian city Lagos on Sunday had 147 people on board, a source at the national emergency management agency said. The source said the aircraft belonged to privately owned domestic carrier Dana Air. Two sources at Lagos airport also said the number on board was around 150. REUTERS/Stringer (NIGERIA - Tags: DISASTER TRANSPORT) QUALITY FROM SOURCE
Ajali ya ndege NigeriaPicha: Reuters

Rais Jonathan ameyasema hayo wakati alipolitembelea eneo la kitongoji cha mji wa Lagos, ambako ndege ya abiria ya shirika la Dana ilianguka jana na kuwaua abiria wote 153 waliokuwemo katika ndege hiyo.

"Tumekuwa tukijizatiti kuboresha sekta ya usafiri wa ndege hapa nchini. Ajali hii ni pigo kubwa kwetu na nitahakikisha ajali kama hii haitokei tena humu nchini," amesena rais Jonathan baada ya kujionea kwa macho yake uharibifu uliosababishwa na kuanguka kwa ndege hiyo.

©Jonathan Rebboah/Wostok Press/Maxppp France, Paris 25/11/2011 Le president du Nigeria Goodluck Jonathan arrive au palais de l Elysee The President of Nigeria Goodluck Jonathan at the Elysee Palace
Rais wa Nigeria, Goodluck JonathanPicha: picture alliance / dpa

Waziri wa usafiri wa ndege nchini Nigeria, Stella Oduah- Ogiemwonyi amesema serikali inafanyika kila linalowezekana kuepusha ajali kama hiyo katika siku zijazo. "Serikali itafanya uchunguzi wa kina kubaini kilichotokea. Hatufahamu chanzo cha ajali, lakini tunafahamu ndege ilikaribia kutua kabla marubani kuonya walikabiliwa na matatizo."

Uchunguzi watatizwa

Polisi wamefyetua gesi ya kutoa machozi kuutawanya umati wa watu waliokusanyika katika eneo la ajali. Kwa mujibu wa taarifa ya mwandishi wa habari wa shirika la AFP, polisi walilazimika kutumia vitoa machozi wakati watu takriban 2,000 walipojaribu kuingia eneo lililofungwa na polisi wakitaka kushuhudia athari za ajali hiyo na hivyo kutatiza uchunguzi.

Kufikia sasa waokoaji wamefaulu kuzitoa maiti zisizopungua 62 kutoka kwa mabaki ya ndege hiyo. Kanisa, jengo la makaazi ya watu la ghorofa mbili na duka la huduma za uchapishaji liliharibiwa vibaya katika eneo la ajali. Idadi kamili ya watu waliokufa ardhini hadi sasa haijajulikana. Moshi ungali unafuka katika eneo la ajali na malori ya zimamoto yamekuwa mbioni kuuzima moto unaoendelea kuwaka kwenye mabaki ya ndege hiyo.

Solomon Omotayo ni miongoni mwa watu walioshuhudia ndege ya shirika la Dana ikipoteza muelekeo muda mfupi kabla kuanguka katika kitongoji cha Iju jijini Lagos. "Tulipoiona, ilkuwa chini mno! Dakika kama mbili baadaye tukasikia mlio. Tuliufuata moshi hadi hapa. Maafisa waliondoa maiti lakini sijui ni ngapi. Ni hasara kubwa na maiti nyingi zingali zimefunikwa."

Emergency workers and volunteers hose down wreckage at the scene of a plane crash in Nigeria's commercial capital Lagos, June 3, 2012. A passenger plane carrying nearly 150 people crashed into a densely populated part of Lagos on Sunday, in what looked like a major disaster in Nigeria's commercial hub. There was no early word from airline or civil aviation authority officials in the West African country on casualties. REUTERS/Stringer (NIGERIA - Tags: DISASTER TRANSPORT TPX IMAGES OF THE DAY) QUALITY FROM SOURCE
Mabaki ya ndege iliyoanguka LagosPicha: Reuters

Shirika la safari za ndege lawamani

Mtaalamu wa safari za ndege nchini Nigeria, Rubani Mohammed Jibrin amelishutumu shirika la safari za ndege kwa rushwa usimamizi mbaya. "Ukweli ni kwamba shirika la usafiri wa anga nchini Nigeria halitimizi wajibu wake. Kuna mambo mengi yanayokwenda kombo katika shirika hilo. Kuna rushwa na ukweli unafichwa. Utoaji mafunzo na kusainiwa kwa mikataba hakufanyiki kwa njia sahihi. Ununuzi na uagizaji wa ndege kutoka nje unafanywa kiholela."

Rubani Mohammed Jibrin amemnyoshea kidole cha lawama mkurugenzi mkuu wa shirika la ndege la Nigeria Harold Demuren na kumtaka ajiuzulu mara moja ili kutoa nafasi kwa mtu mwingine aliye tayari kufanya kazi nzuri achukue nafasi yake.

Kwa upande mwingine, mkurugenzi mkuu Harold Demuren, amethibitisha kuwa rubani wa ndege hiyo alikuwa raia wa Marekani akisaidiwa na rubani mwenzake raia wa India.

Mwandishi: Josephat Charo/AFPE/DPAE/APE

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman