1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Obama hataonana na Rowhani New York

21 Septemba 2013

Rais Barack Obama wa Marekani hana mipango ya kukutana na rais wa Iran Hassan Rowhani kujadili mgogoro wa taifa hilo kuhusu mpango wake wa nyuklia, pembezoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

https://p.dw.com/p/19lQa
Hassan Rowhani, moderate presidential candidate and former top nuclear negotiator, addresses an electoral campaign event in northern Tehran on May 30, 2013. Rowhani, the only cleric in the race, says his experience in leading talks with the so-called P5+1 group -- the United States, Russia, China, France, Britain plus Germany -- could help resolve the nuclear standoff. AFP PHOTO/BEHROUZ MEHRI (Photo credit should read BEHROUZ MEHRI/AFP/Getty Images)
Rais wa Jamhuri ya Iran Hassan RowhaniPicha: Behrouz/AFP/Getty Images

Uvumi kuhusu kuwepo mkutano huo unamuhusu kiongozi huyo aliyeingia madarakani Agosti mwaka huu, ambae amejieleza kutaka kujihusisha zaidi na mataifa ya magharibi zaidi ya mtangulizi wake Mahmoud Ahmadinejad umetoweka.

Naibu mshauri wa masula ya usalama, Ben Rhodes amesema "kilichopo ni kujihusisha kwa uwazi kabisa na Iran lakini kwa msisitizo maneno yao yafuatane na vitendo". Aidha alibainisha kwamba kwa mara kadhaa rais Obama ameacha milango wazi ya mazungumzo na Wairan. Obama na Rowhani kwa pamoja wamepangwa kuzungumza Jumanne ijayo huko makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York.

(L-R) US President Barack Obama, Defense Secretary Chuck Hagel and Joint Chiefs Chairman Gen. Martin Dempsey pay their respects at the Pentagon Memorial to mark the 12th anniversary of the 9/11 attacks on the South Lawn of the White House in Washington, DC, on September 11, 2013. AFP PHOTO/Jewel Samad AFP PHOTO / Jewel Samad (Photo credit should read JEWEL SAMAD/AFP/Getty Images)
Rais Barack Obama wa Marekani, Waziri wa Ulinzi Chuck HagelPicha: AFP/Getty Images

Aidha Obama atakutana na Rais Mahmoud Abbas pembezoni mwa mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza tangu kuanza upya mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina.

Tatizo la wakimbizi wa Syria

Mkutano huo wa Jumanne unafanyika kabla ya ule wa uliyopangwa na Ikulu ya Marekani, unaomuhusu Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu Septemba 30. Obama vilevile atakutana na Rais wa Lebanon Michel Suleiman kujadili wimbi la wakimbizi kutoka nchi jirani ya Syria.

Syrian refugees take part in a demonstration at the Zaatari refugee camp, near the border with Syria, calling for the international community to arm the rebel Free Syrian Army on February 22, 2013. Jordan says it is hosting around 380,000 Syrian refugees, including some 83,000 in Zaatari, which has seen frequent protests, mainly over poor living conditions. AFP PHOTO / KHALIL MAZRAAWI (Photo credit should read KHALIL MAZRAAWI/AFP/Getty Images)
Wakimbizi wa Syria wakiwa katika kambi ya Zaatari, nchini Jordan wakiwa wamekusanyika kuomba jumuiya ya kimataifa kuwasaidiaPicha: Getty Images

Vilevile intarajiwa atakutana na rais wa Nigeria Goodlulc Jonathan, kuzungumzia jitihada za kukuza uchumi barani Afrika na ushirikiano wa usalama katika kukabiliana na wanamgambo wa kundi la waislamu wenye itikadi kali Boko Haram.

Rowhani kuzungumza na Hollande

Kwa kutumia mtandao wake wa twitter Ijumaa, Rowhani amesema atakutana na rais wa Ufaransa Fracois Hollande. Na rais Omar al-Bashir wa Sudan anaetafutwa na mahakama ya uhalifu ICC, kutokana na uhalifu wa kivita na mauwaji ya halaiki, amepangwa kuzungumza Ijumaa katika mkutano huo wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa. Wanaharakati wa haki za binadaamau wamelaani kiongozi huyo kuiwakilisha Sudan katika mkutano huo mkubwa wa kimataifa.

Kwa upande wake Marekani ilikataa kuzungumza chochote iwapo Bashir anapewa visa ya kuingia nchini humo au la. Pamoja na kuwepo kwa utata wa kisheria wa rais huyo lakini Marekani kama taifa mwenyeji wa Baraza kuu la Umoja wa mataifa inapaswa kuruhusu wakuu wote wamataifa kuhudhuria mkutano huo.

Mwandishi: Sudi Mnett DPA

Mhariri: Sekione Kitojo.