PARIS : Taasisi za magharibi zakata uhusiano na ile ya Iran
17 Desemba 2006Matangazo
Takriban taasisi za utafiti 40 za Ulaya na Marekani ya Kaskazini zimesema kwamba zinasitisha mawasiliano na jopo kuu la ushauri la Iran ambalo limesaidia kuandaa mkutano wa wiki iliopita mjini Tehran wa watu wanaokanusha Maangamizi ya Wayahudi. Taasisi hizo zimekubali kusitisha mipango inayoendelea kutekelezwa na Taasisi ya Masomo ya Kisiasa ya Kimataifa ya Iran.
Mkutano uliofanyika tarehe 11 na 12 mwezi huu wa Desemba mjini Tehran uliwajumuisha pamoja watu wanaokanusha Maangamizi ya Wayahudi kutoka duniani kote kujadili iwapo au la mauaji ya kimbari ya Wayahudi milioni sita yametokea kweli wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.