1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

PARIS:serikali mpya kuundwa nchini Ufaransa

19 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBqU

Rais Nicolas Sarkozy wa Ufaransa amemwagiza waziri wake mkuu bwana Francois Fillon kuunda serikali mpya baada ya chama cha kihafidhina cha rais huyo kushinda katika uchaguzi wa bunge mwishoni mwa wiki iiyopita. Chama cha rais Sarkozy kilishinda kwa kupata viti 314 katika bunge lenye viti 577.

Rais huyo amesema atatumia fursa inayotokana na ushindi huo kutekeleza mageuzi aliyowaahidi wananchi wake, ikiwa pamoja na kuweka sheria ngumu za uhamiaji, kupunguza kodi na kurekebisha mfumo wa afya uliolemewa na deni.