1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

PARIS:Uchaguzi wa wabunge waendelea Ufaransa

10 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBt3

Wananchi wa Ufaransa wanapiga kura katika duru ya mwanzo kuwachagua wabunge huku chama cha rais Nicolas Sarkozy cha UMP kikitarajiwa kujiimarisha madarakani.

Sarkozy aliyechaguliwa kuwa rais wa Ufaransa mwezi mmoja uliopita kwa kunadi sera za kufanya mageuzi nchini humo anahitaji kupata ushindi wa bunge baada ya duru ya pili ya uchaguzi wa bunge mnamo juni 17 ili kufanikisha mageuzi anayoyataka.

Uchaguzi wa bunge pia unafanyika nchini Ubelgiji ambako uchunguzi wa maoni unaonyesha chama cha upinzani cha Christian Demokrats kitashinda dhidi ya waliberali.