1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

"Pasaka ni Machipuko "wanasema viongozi wa kidini nchini Ujerumani

8 Aprili 2007
https://p.dw.com/p/CCBJ

Mainz-Berlin:

Mwenyekiti wa baraza la maaskofu wa Ujerumani,Kardinal Karl Lehmann akihubiri wakati wa misa ya Pasaka ametoa mwito “wapatiwe fursa mpya hata wale waliofanya makosa yaliyofurutu.””Waliopotoka hawastahiki watu kuwakatia tamaa” amesema Kardinal Lehmann alipokua akihutubia misa katika kanisa kuu la Mainz. Mwenyekiti wa baraza kuu la kanisa la kiinjili Askofu Wolfgang Huber amesema kwa upande wake tunanukuu:”Sherehe za Pasaka ni dalili ya machipuko.Kutokana na imani zao za kidini,binaadam wanaweza ku kuepukana na hofu na hali ya akukata tamaa”-mwisho wa kumnukuu askofu Wolfgang Huber,aliyesema hayo katika misa ya pasaka katika kanisa kuu la mjini Berlin.