PHUKET:Thailand yasema rubani angeweza kuepuka ajali
18 Septemba 2007Matangazo
Maafisa wa usalama wa anga nchini Thailand wamesema kuwa rubani wa ndege iliyopata ajali siku ya jumapili alipata ruhusa ya kutua muda mfupi tu kabla ya ajali hiyo iliyoua watu 89.
Wamesema kuwa ndege mbili zilizotua muda mfupi kabla ya ndege hiyo zilitoa taarifa ya hali ya upepo mkali kitu ambacho rubani angeweza kukiepuka.
Waziri wa usafiri wa Thailand amewataka wananchi kutohukumu kabla ya uchunguzi kukamilika.
Taarifa za safari za ndege hiyo zinatarajiwa kupelekwa Marekani na majibu yanatajiwa mnamo ndani ya kipindi cha wiki mbili.