1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi Ujerumani yawatia mbaroni washukiwa wa ugaidi

Isaac Gamba
1 Februari 2017

Polisi nchini Ujerumani imewakamata watu watatu wakihusishwa na  kundi la itikadi kali linalojiita Dola la Kiislamu. Ni katika harakati zinazoendelea kuwagundua wanaopanga njama za kufanya mashambulio.

https://p.dw.com/p/2Wldj
Deutschland Sicherheit Sylvester
Picha: Reuters/F. Bensch

Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kuwa washukiwa hao walikuwa wanapanga shambulizi kubwa la kigaidi.  Aidha polisi walivamia msikiti mmoja ulioko katika eneo la  Moabit mjini Berlin ambako watu hao wanadaiwa kuwa walikuwa wakikutana kwa mazungumzo. Watu 12 waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa Desemba 19 mwaka jana  katika shambulizi linalodaiwa kufanywa na raia mmoja wa Tunisia Anis Amri  baada ya kuendesha lori katika soko la Krismasi mjini Berlin lililokuwa limefurika watu hali iliyopelekea serikali ya Ujerumani kuchukua hatua za kuimarisha usalama.

Mwandishi: Isaac Gamba/dw

Mhariri: Gakuba Daniel