1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Purukushani zaigubika Ugiriki

20 Oktoba 2011

Mamia ya vijana wameyavamia na kuyapora maduka katikati ya mji mkuu wa Ugiriki wa Athens, walipopambana na polisi wa kuzuwia ghasia.

https://p.dw.com/p/12vag
Waziri Mkuu wa Ugiriki,George PapandreouPicha: dapd

Purukushani hizo zilitokea pindi baada ya bunge la Ugiriki kuiidhinisha miswada mipya itakayoiwezesha serikali kubana matumizi kwa kiasi kikubwa zaidi. Hata hivyo, miswada hiyo inasubiri kuidhinishwa rasmi katika kura ya pili itakayopigwa hii leo.

George Papandreou Griechenland Krise Flash-Galerie
Wafuasi wa chama tawala cha Kisoshalisti wakiandamana: Raia wa Ugiriki wanazipinga hatua za kubana matumizi kwa kiasi kikubwa zaidi.Picha: dapd

Mgomo na Mikato

Vurumai hizo za Jumatano jioni zilitokea wakati ambapo mgomo wa kitaifa utakaodumu kwa muda wa saa 48 ulipokuwa ukianza. Taarifa zinaeleza kuwa huduma muhimu zilikwamishwa kote nchini Ugiriki kwasababu ya mgomo huo.

Kulingana na miswada hiyo mipya, raia wa Ugiriki watalazimika kulipa kodi zaidi, kupunguziwa malipo yao ya uzeeni pamoja na mishahara, kadhalika kusimamishiwa kwa muda malipo ya mishahara iliyopunguzwa ya wafanyakazi alfu 30 vilevile kuisitisha mikataba mipya.

Griechenland Athen Parlament Papandreou Krise Finanzkrise Flash-Galerie
Bunge la Ugiriki: Kura ya pili kupigwa leo(20.10.2011) kuziidhinisha sheria za kubana matumizi kwa kiasi kikubwa zaidi.Picha: picture alliance/dpa

Punguzo kwa kila sekta

Serikali ya Ugiriki imelazimika kuichukua hatua hiyo kabla ya kupokea mikopo zaidi kati ya fungu la euro bilioni 110 ilizoahidiwa na serikali za mataifa ya Ulaya pamoja na Shirika la Fedha Ulimwenguni, IMF. Kwa upande wake, uongozi wa Ugiriki umesisitiza kuwa hautakuwa na fedha zozote endapo hautopokea kiasi ya euro bilioni 8 za mwanzo, jambo linalopingwa na Wagiriki. Waziri wa Fedha wa Ugiriki, Evangelos Venizelos anashikilia kuwa suluhu ni kukabiliana na hali hiyo ngumu.

Mwandishi: Mwadzaya, Thelma-ZPR

Mhariri: Mtulya, Abdul