1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Kabila atangazwa mshindi wa uchaguzi DRC

10 Desemba 2011

Tume ya uchaguzi katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, imemtangaza rais wa sasa Joseph Kabila kuwa amechaguliwa tena kwa asilimia 49 ya kura .

https://p.dw.com/p/13QH6
kabila.jpg **FILE** President Joseph Kabila smiles during a meeting with former heads of state in Kinshasa, Congo in this Saturday, Nov. 4, 2006 file photo. Kabila appeared to have an insurmountable lead Tuesday, Nov. 14, 2006, in Congo's runoff election with nearly all the votes counted. (AP Photo/Schalk van Zuydam, FILE)
Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya CongoPicha: AP Photo

Tume hiyo imesema kuwa mgombea wa karibu ya Kabila, kiongozi wa upinzani Etienne Tshsekedi , amepata asilimia 32 ya kura. Watu waliojitokeza kupiga kura katika nchi hiyo kubwa barani Afrika ni asilimia 59.
Tshisekedi amekataa matokeo hayo na kujitangaza kuwa rais mteule. Mahakama kuu katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo inapaswa hadi tarehe 17 mwezi huu kusikiliza rufaa za uchaguzi huo. Wakati matokeo yakitangazwa mjini Kinshasa jana Ijumaa, waungaji mkono wa rais Kabila walishangiria lakini wafuasi wa Tshisekedi wameeleza kuwa na hali ya wasi wasi. Ghasia wakati wa uchaguzi wa hapo Novemba 28 zimesababisha watu 18 kuuawa na kusababisha baadhi ya wakaazi kuikimbia nchi hiyo. Wachunguzi wa kimataifa wamesema kuwa uchaguzi huo umekumbwa na mapungufu kadha lakini wameshindwa kuuita wa udanganyifu. Matokeo ya awali ya uchaguzi wa bunge yanatarajiwa ifikapo katikati ya mwezi wa Januari. Rais ataapishwa Desemba 20.


DR Congo elections epa03017273 Top opposition leader Etienne Tshisekedi (C) arrives for a news conference at his residence in Kinshasa, the Democratic Republic of Congo, 27 November 2011. The veteran politician vowed to hold a public rally, defying a government order banning political rallies after at least three people had reportedly been killed in a clash on previous day. Presidential and parliamentary elections are scheduled to be held in DR Congo on 28 November 2011 amid concerns over the prospects for fair elections. Tshisekedi, a 78-year-old opposition leader and the head of the Union for Democracy and Social Progress (UDPS), and Vital Kamerhe, a former UDPS member, are among many others who are challenging incumbent Joseph Kabila in the country's second election since the end of a bloody civil war in 2003. Election-related violence has already broken out in parts of the country ahead of the poll. Election official has said on 27 November that there will be no delay and elections will go as planned on 28 November, despite concerns by many that it would be delayed due to the violence and logistical difficulties in the country two-thirds the size of Western Europe. EPA/DAI KUROKAWA
Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo Etienne TshisekediPicha: picture-alliance/dpa