1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa mpito aapishwa Tunisia

Sekione,Kitojo/ZPR16 Januari 2011

Rais wa mpito ameapishwa nchini Tunisia na amemuomba waziri mkuu, kuunda serikali ya umoja wa kitaifa, ikijumuisha pia wajumbe kutoka vyama vya upinzani.

https://p.dw.com/p/QshB
Rais wa mpito wa Tunisia, Fouad MebazaaPicha: AP
Spika wa zamani wa bunge la Tunisia, Fouad Mebazaa amechukua wadhifa wa rais wa mpito, kufuatia rais wa zamani Zine al Abidine Ben Ali, kukimbilia nchini Saudi Arabia. Baada ya mwezi mzima wa ghasia, kumekuwa na uporaji na milio ya risasi ilisikika katika mji mkuu Tunis, huku wanajeshi wakiwa na vifaru wakifanya doria katika mitaa ya mji huo. Karibu watu 50 wanaripotiwa kuwa wameuwawa katika ghasia zilizotokea katika jela moja. Rais wa mpito Mebazaa, ametoa wito wa kutaka utulivu. Baraza la Katiba la Tunisia, limesema kuwa uchaguzi mpya utafanyika katika muda wa siku 60, licha ya viongozi wa upinzani kusema kuwa muda zaidi unahitajika.
German Chancellor Angela Merkel gestures during a joint press conference with French President Nicolas Sarkozy, not seen, at the Elysee Palace in Paris, Thursday, Jan. 8, 2009. French President Nicolas Sarkozy hit out Thursday at financial speculators for having "perverted" capitalism, which he said should be overhauled with a new role for governments and moral values. Speaking alongside German Chancellor Angela Merkel and former British Prime Minister Tony Blair at a conference on the future of global finances in Paris, Sarkozy criticized "an immoral system where the logic of the markets excuses everything, where money follows money." (AP Photo/Michel Euler)
Kansela wa Ujerumani, Angela MerkelPicha: AP

Wakati huo huo, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, amewataka Watunisia kuanzisha kile alichokiita demokrasia ya kweli na ameongezea kuwa Umoja wa Ulaya pia utaunga mkono kile alichokiita mwanzo mpya. Ufaransa, mshirika wa zamani wa rais aliyeondolewa madarakani, Ben Ali, imetoa wito wa kufanywa uchaguzi huru nchini Tunisia haraka iwezekanavyo. Nae Muammar Gaddafi, kiongozi wa Libya iliyo jirani ya Tunisia, amesema kuwa anasikitishwa na kuanguka kwa Ben Ali kutoka madarakani.