1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Somalia amelazwa hospitali Kenya

5 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CXQf

Rais wa Somalia,Abdullahi Yusuf amelazwa hospitali mjini Nairobi huku habari zikitatanisha kuhusu hali yake.Balozi wa Somalia nchini Kenya, Mheshimiwa Mohamed Ali Nur amesema,Rais Yusuf anafanyiwa uchunguzi wa kawaida kabla ya kuelekea London.Wakati huo huo,alikanusha habari zilizosema kuwa hali ya kiongozi huyo ni mbaya.