1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Ujerumani kuanza ziara nchini Uturuki

22 Aprili 2024

Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier ataanza hii leo ziara yake nchini Uturuki, ili kudhihirisha uhusiano wa karibu kati ya mataifa hayo mawili.

https://p.dw.com/p/4f289
Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier
Rais wa Ujerumani Frank-Walter SteinmeierPicha: Jan Woitas/dpa/picture alliance

Steinmeier ambaye anazuru Uturuki kwa mara ya kwanza tangu awe rais, amekuwa na mitazamo tofauti na kiongozi wa Uturuki Tayyip Erdogan.

Rais huyo wa Ujerumani alikosoa msimamo wa serikali ya Erdogan kuhusu Israel na pia aliwahi kuibua wasiwasi wake kuhusu mmomonyoko wa  kanuni za kidemokrasia nchini Uturuki.

Kituo cha kwanza cha ziara yake itakuwa mji wa Istanbul, ambapo atakutana na wanaharakati wa mashirika ya kiraia, pamoja na meya wa jiji hilo, kiongozi wa upinzani Ekrem Imamoglu, na kisha kukutana na manusura wa tetemeko kubwa la ardhi la mwaka jana huko Gaziantep karibu na mpaka wa Syria. Siku ya Jumatano, Steinmeier anatarajiwa kukutana na Erdogan mjini Ankara.