ROM: Blair amekutana na Papa Benedikt XVI
23 Juni 2007Matangazo
Waziri Mkuu wa Uingereza Tony Blair,amekutana na Papa Benedikt XVI.Kwa mujibu wa Vatikan,mada zilizojadiliwa ni mgogoro wa Mashariki ya Kati na mustakabali wa Umoja wa Ulaya.Mkutano huo wa faragha umefanywa,wakati kukivuma kuwa Blair anataka kuingia katika dini ya Katoliki.