1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda: Uwezekano wa Jenerali Bosco Ntaganda kupelekwa ICC upo?

21 Machi 2013

Marekani inaangalia uwezekano wa kumpeleka Jenerali Bosco Ntaganda kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC.

https://p.dw.com/p/181Cv
Jenerali Bosco Ntaganda
Jenerali Bosco NtagandaPicha: dapd

Serikali ya Marekani imesema kwamba wanasheria kutoka mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC wako njiani kuelekea mjini Kigali Rwanda kuangalia uwezekano wa kumpeleka the Hague Jenerali Bosco Ntaganda aliyesajilimisha siku ya Jumatatu kwenye ubalozi mjini Kigali.Naibu waziri wa Marekani anayehusika na Afrika Johnnie Carson amesema bado hakuna uhakika wa ni siku gani Bosco Ntaganda atapelekwa ICC. Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylvanus Karemera anaripoti zaidi na ili uweze kuisikiliza bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mwandishi: Sylvanus Karemera

Mhariri: Mohamed Abdul-Rahman