1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Safari hii Ghana inalenga kutamba

9 Juni 2014

Ghana wametambulika kama mojawapo ya timu bora zaidi za soka barani Afrika kwa miaka kadhaa sasa, baada ya kudhihirisha mchezo wa hali ya juu katika Kombe la Dunia mwaka wa wa 2006 na 2010.

https://p.dw.com/p/1CF4A
Interaktiver WM-Check 2014 Mannschaft Ghana
Picha: picture alliance/AP

The Black Stars wanataraji angalau kufuzu katika awamu ya mwondowano kwa mara ya tatu mfululizo katika dimba la mwaka huu. Ghana iliibaza Jamhuri ya Czech na Marekani katika Kombe la Dunia mwaka wa 2006 nchini Ujerumani, kanla ya kuzidiwa nguvu na mabingwa mara nyingi Brazil katika raundi ya 16 bora. Nchini Afrika Kusini, Black Stars walikuwa timu pekee ya Afrika kufuzu kutoka awamu ya makundi. Waliizaba Marekani tena kabla ya kuzidiwa nguvu na Uruguay kupitia mikwaju ya penalty katika robo fainali. Licha ya kufanya vibaya katika Kombe la Mataifa ya Afrika, maafisa wa soka nchini humo waliamua kusalia na kocha James Kwesi Appiah.

Barabara ya kufika Brazil ilikuwa na changamoto lakini Ghana iliweza kuwapiku Misri katika mechi ya mchujo. Vijana hao kama wangepenga kufanya vyema nchini Brazil, watahitaji mchezo mzuri kutoka kwa wachetaji wake kama vile Michael Essien wa AC Milan, Kwadwo Asamoah wa Juventus, Kevin-Prince Boateng wa Schalke na Asamoah Gyan.

Wapinzani wa Ghana katika Kundi G ni Ujerumani, Ureno na Marekani.

Mwandishi: Bruce Amani/dpa
Mhariri: Yusuf Saumu