1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SAN DIEGO: Rais Bush atembelea eneo la maafa

26 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7Ch

Rais wa Marekani,George W.Bush ametembelea jimbo la Kalifornia kujionea mwenyewe hasara iliyosababishwa na mioto.Bush alikuwa pamoja na Gavana wa Kalifornia,Arnold Schwarzenegger.Karibu na mji wa San Diego,zaidi ya nyumba 8,500 zipo hatarini.Hadi hivi sasa si chini ya watu 500,000 wamelazimika kuondoka majumbani mwao.