1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Serikali ya Kongo yapinga Chebeya kuzikwa Juni 30 mwaka huu

Josephat Nyiro Charo18 Juni 2010

Juni 30 ni siku ya kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa Kongo

https://p.dw.com/p/Nwtr
Marehemu Floribert ChebeyaPicha: picture-alliance/ dpa/dpaweb

Mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu, Floribert Chebeya, ambaye alipatikana amekufa akiwa ndani ya gari lake mjini Kinshasa hapo tarehe 2 mwezi huu, atazikwa Jumamosi, tarehe 26 mwezi huu.

Mpango wa mazishi unafuatia hatua ya mwendesha mashataka mkuu wa taifa kuirejesha maiti ya Chebeya kwa familia yake baada ya kufanyiwa uchunguzi wiki iliopita na madaktari kutoka Uholanzi.

Hata hivyo, mashirika ya kutetea haki za binadamu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo yameomba mazishi ya Floribert Chebeya yafanyike Juni 30, siku ambayo nchi hiyo itaadhimisha miaka 50 ya uhuru wake.

Taarifa kamili na mwandishi wetu wa Kinshasa, Saleh Mwanamilongo

Mwandishi, Saleh Mwanamilongo

Mpitiaji, Peter Moss

Mhariri, Othman Miraji