1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shelly-Ann Fraser-Pryce achukua dhahabu ya mita 100

25 Agosti 2015

Mwanariadha wa Jamaica Shelly-Ann Fraser-Pryce alitimka kwa kasi na kutwaa medali ya dhahabu katika mbio za mita 100 kwa upande wa wanawake kwenye mashindano ya riadha ya dunia yanayoendelea Beijing, China

https://p.dw.com/p/1GKwf
China, Shelly-Ann Fraser-Pryce Leichtathletik WM
Picha: Getty Images/A. Lyons

Ilikuwa ni dhahabu ya sita kwa mwanariadha huyo kushinda baada ya kushinda mbio za mita 100 na 200 mwaka 2013.

Schippers ni bingwa wa mbio za Heptathlon baada ya kushinda medali ya shaba miaka miwili iliopita.

Ni rekodi ya taifa kwa upande wa Schippers ambaye alianza kushiriki katika mbio fupi mnamo mwezi Juni huku Bowie mwenye umri wa miaka 24 akinyakua taji lake kuu la kwanza.

Mwanariadha wa Nigeria aliyepigiwa upatu kufanya vizuri Blessing Ogakbare alishika mkia katika mbio hizo.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP
Mhariri: Sekione Kitojo