1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Soka: Werder Bremen juu kileleni.

10 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCkp

Mlinzi kutoka Brazil Naldo ameweka wavuni mabao matatu wakati Werder Bremen ikirejea kileleni katika ligi ya Ujerumani Bundesliga, baada ya kutolewa katika kinyang’anyiro cha kombe la ligi ya mabingwa , Champions League, na kuikung’uta Eintracht Frankfurt kwa mabao 6-2.

Ushindi huo mjini Frankfurt umeifikisha Bremen katika point 33, point mbili zaidi ya VFB Stuttgart ambao walipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Buchum, wakati mabingwa watetezi Bayern Munich walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ernegie Cottbus