1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Soko la kale laungua moto Aleppo

30 Septemba 2012

Mamia ya maduka yameungua moto katika soko la kale mjini Aleppo Jumamosi(29.09.2012)wakati mapigano baina ya waasi na majeshi ya serikali, yanatishia kuharibu eneo hilo lililotengwa na UNESCO kuwa turathi ya dunia.

https://p.dw.com/p/16HeL
In this image taken from video obtained from Shaam News Network (SNN), which has been authenticated based on its contents and other AP reporting, a fire rages at a medieval souk in Aleppo, Syria. Syrian rebels and residents of Aleppo struggled Saturday to contain a huge fire that destroyed parts of the city's medieval souks, or markets, following raging battles between government troops and opposition fighters there, activists said. Some described the overnight blaze as the worst blow yet to a historic district that helped make the heart of Aleppo, Syria's largest city and commercial hub, a UNESCO world heritage site. (Foto:Shaam News Network SNN via AP video/AP/dapd)
Soko la kale likiungua mjini AleppoPicha: AP

Vuguvugu la mageuzi lililogeuka kuwa vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vinaendelea hivi sasa nchini Syria vimesababisha watu 30,000 kupoteza maisha yao, kwa mujibu wa makundi ya wanaharakati nchini Syria kama kundi linaloangalia haki za binadamu nchini humo lenye makao yake makuu mjini London.

Lakini mbali na gharama ya upotevu wa maisha ya watu , lakini nyingi ya hazina za kihistoria pia zimeharibiwa katika mzozo huo uliodumu sasa miezi 18, ambao umeyaacha baadhi ya maeneo ya miji kuwa magofu.

In this image taken from video obtained from Shaam News Network (SNN), which has been authenticated based on its contents and other AP reporting, a fire rages at a medieval souk in Aleppo, Syria. Syrian rebels and residents of Aleppo struggled Saturday to contain a huge fire that destroyed parts of the city's medieval souks, or markets, following raging battles between government troops and opposition fighters there, activists said. Some described the overnight blaze as the worst blow yet to a historic district that helped make the heart of Aleppo, Syria's largest city and commercial hub, a UNESCO world heritage site. (Foto:Shaam News Network SNN via AP video/AP/dapd)
Soko ambalo ni turathi za dunia mjini Aleppo likiungua motoPicha: AP

Mashambulio mapya mjini Aleppo

Wapiganaji wanaopigana kumwondoa madarakani rais Bashar al-Assad wametangaza kuwa wamefanya shambulio jipya dhidi ya mji wa Aleppo, mji wa kibiashara wa Syria wenye wakaazi wapatao milioni 2.5, siku ya Alhamis, lakini hakuna upande unaoonekana kupata ushindi.

Mjini Aleppo , wanaharakati wakizungumza kupitia mtandao wa Skype wamesema wanajeshi wa serikali waliokaa katika maeneo maalum wakiwalenga watu shabaha, wanafanya hali kuwa ngumu kwa wao kukaribia eneo la Souk al-Madina, soko la kale lenye njia nyembamba lililoko katika mji mkongwe, ikiwa ni moja kati ya vivutio vikubwa vya utalii.

GettyImages 152915254 A picture taken on September 28, 2012 shows damaged vehicles and buildings in the northern city of Aleppo following months of clashes and battles between Syrian rebels and government forces. AFP PHOTO/MIGUEL MEDINA (Photo credit should read MIGUEL MEDINA/AFP/GettyImages)
Mapigano yameacha baadhi ya maeneo kuwa magofu mjini AleppoPicha: Getty Images

Soko laungua

Video vizilizowekwa katika tovuti ya You Tube katika mtandao wa internet , zinaonesha wingu kubwa jeusi likitanda katika anga la mji huo.

Wanaharakati wamesema kuwa moto umezuka kutokana na mashambulio ya makombora na risasi siku ya Ijumaa na wanakadiria kuwa kati ya maduka 700 hadi 1,000 yameharibiwa hadi sasa. Maelezo hayo ni vigumu hata hivyo kuweza kuthibitishwa, kwasababu serikali inazuwia vyombo vya habari vya kimataifa.

GettyImages 152898942 Syrian rebel fighters take their position during fighting with government troops in the old city of Aleppo on September 28, 2012. Syrian rebels advanced on several fronts in their campaign to seize Aleppo, but without a significant breakthrough after hours of fierce fighting, commanders in the northern city told AFP. AFP PHOTO/MIGUEL MEDINA (Photo credit should read MIGUEL MEDINA/AFP/GettyImages)
Wapiganaji wa jeshi la waasi mjini AleppoPicha: Getty Images

Mji mkongwe uliopo mjini Aleppo ni moja kati ya maeneo yaliyotengwa na shirika la umoja wa mataifa ya sayansi na utamaduni UNESCO, kuwa turathi ya dunia, ambapo hivi sasa umo katika hatari kutokana na mapigano hayo.

Maeneo mengine hatarini

UNESCO inaamini kuwa maeneo matano kati ya sita ya turathi nchini Syria , ambayo pia ni pamoja na mji wa kale uliopo jangwani wa Palmyra na sehemu za mji mkongwe mjini Damascus yameathirika.

A Free Syrian Army sniper aims his weapon at his position at the Bustan Al-Basha front line in southeastern Aleppo September 18, 2012. REUTERS/Zain Karam (SYRIA - Tags: CONFLICT CIVIL UNREST POLITICS)
Mapigano yakiendelea nchini SyriaPicha: Reuters

Shirika la kuangalia haki za binadamu nchini Syria lenye makao yake makuu mjini London , ambalo linamtandao wake wa wanaharakati nchini Syria , limesema kuwa majeshi ya Assad na waasi wanalaumiana kila mmoja kwa kuzusha moto huo.

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre

Mhariri: Bruce Amani