STOCKHOLM : Bastola yahusishwa na mauaji ya Palme
21 Novemba 2006Matangazo
Polisi ya Sweden imegunduwa bastola inayohusishwa na mauaji ya Waziri Mkuu Olof Palme hapo mwaka 1986.
Bastola hiyo imepatikana kwenye ziwa katikati ya Sweden hata hivyo polisi imesema ni mapema mno kusema iwapo hiyo ndio ilikuwa silaha halisi ya mauaji ambayo imepelekwa kufanyiwa uchunguzi kwenye maabara.Afisa alieko kwenye timu ya uchunguzi huo amesema uchunguzi umeonyesha kwamba risasi kutoka kwenye bastola hiyo ambayo ilitumiwa kwa ajili ya wizi hapo mwaka 1983 inafanana na zile zilizopatikana katika eneo la mauaji ya Palme.
Mauaji ya kiongozi huyo wa Sweden hadi leo yamekuwa kitendawili ambapo sio muuaji wala silaha iliotumika kwa mauaji hayo vimeweza kupatikana katika uchunguzi unaoendelea.