1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tanzania, katiba mpya na Muungano

11 Juni 2013

Baada ya Tume ya Katiba chini ya uwenyekiti wa Jaji Joseph Sinde Warioba kuiweka hadharani rasimu ya katiba hiyo, sasa maswali mengi yameanza kuulizwa kwa lengo la kuichambua, mojawapo likiwa ni muundo mpya wa Muungano.

https://p.dw.com/p/18nbG
DW online Karte Tanzania eng karussell
DW online Karte Tanzania eng karussell

Katika kipindi hiki cha Maoni mbele ya Meza ya Duara, Mohammed Abdulrahman wa Idhaa ya Kiswahili ya DW anaongoza mjadala unaowashirikisha Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Valerie Msoka, mwanasiasa mkongwe na mmoja wa waasisi wa hoja ya Muungano wa Serikali Tatu, Njelu Kasaka, mwakilishi wa Mji Mkongwe na mmoja wa watetezi wa Mamlaka Kamili ya Zanzibar, Ismail Jussa, na mbunge wa CHADEMA, John Shibuda.

Kusikiliza mjadala huu, tafadhali bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mhariri: Mohammed Khelef