1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TEHRAN: Wanaharakati wa kike wamekamatwa nchini Iran

5 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCMJ

Zaidi ya wanaharakati 30 wa kike wamekamatwa katika mji mkuu wa Iran Tehran.Wanawake hao walikusanyika nje ya mahakama mjini Tehran, kuwaunga mkono wenzao 5 wanaopigania haki za wanawake.Wanawake hao 5 wamefikishwa mahakamani kwa sababu mwaka jana waliandaa maandamano kupinga sheria ambazo wamesema huwabagua kijinsia.Wanaharakati hao wameshtakiwa kuhatarisha usalama wa taifa na kushiriki katika maandamano yasio halali.