1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tunisia yapata rais mpya

13 Desemba 2011

Mpinzani wa zamani amekuwa rais mpya wa Tunisia. Hapo jana, Bunge la mpito la Tunisia limemchagua daktari na mwanaharakati wa haki za binadamu Moncef Marzouki kushika wadhfa wa urais.

https://p.dw.com/p/13RUN
Meeting with 13 members of the party executives of the Congress for the Republic for determination of their positions to be followed further to the political situation. Members of CFR talks in the office of Moncef Marzouki at the National Assembly during the tractactions of the last crisis with Ennahdha on the coalition government. The points of tension concern the internal regulation of the assembly and the road map and the mini constitution to react the functioning of the state for this year of transition. Tunis, Tunisia, on November 30, 2011. Photo by Nicolas Fauque/ABACAPRES.COM # 300285_005
Moncef MarzoukiPicha: picture alliance/abaca

Marzouki alifungwa 1994 baada ya kumkosoa Ben Ali katika uchaguzi wa rais. Lakini aliachiwa huru miezi minne baadae na kulazimishwa akaishi uhamishoni Ufaransa. Waangalizi wa nchi za magharibi wanamuona Marzouki kama asiyekuwa na msimamo wa kidini na kuweka mambo sawa kwa chama chenye itikadi ya kiislamu ya wasatani cha Tunisia ambacho kwa hivi sasa kinatawala nguvu ya kisiasa nchini humo. Kiongozi huyo atahudumu mwaka mmoja, mpaka pale ambapo katiba mpya itaandikwa na uchaguzi mpya utafanyika.

Mwandishi: Sudi Mnette