1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tuzo ya Haki ya Maisha yaenda kwa Daktari wa DRC

26 Septemba 2013

Daktari Denis Mukwege wa DRC amekuwa mmoja wa washindi wanne wa tuzo ya Haki ya Maisha kutokana na mchango wao katika kuendeleza haki za binaadamu, kuboresha upatikanaji wa chakula na kukabiliana na silaha za kemikali.

https://p.dw.com/p/19onP
Mshindi wa Tuzo ya Haki ya Maisha Daktari Denis Mukwege
Mshindi wa Tuzo ya Haki ya Maisha Daktari Denis MukwegePicha: Stina Berge

Daktari Mukwege ametambuliwa kutokana na kazi yake ya kuwatibu wanawake waliyoathiriwa na vurugu za kingono wakati wa vita, na pia ujasiri wake wa kuzungumzia vyanzo vya vurugu hizo. Dk.Mukwege anaendesha hospitali mjini Bukavu na amekwisha wahudumia wanawake karibu elfu 40 waliobakwa nchini Kongo. Iddi Ssessanga amezungumza na bibi Tereza Mima kutoka Tume ya haki na amani mjini Bukavu kuhusiana na tuzo hii kwa Dk. Mukwege, anaelezea umuhimu wake kwa watu wa Kongo. Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mwandishi: Iddi Ismail Ssessanga

Mhariri: Mohamed Abdul-Rahman