1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Udugu wa Kiislamu wapanga maandamano zaidi

18 Agosti 2013

Wakikaidi ukandamizaji unaofanywa na serikali ya mpito inayoungwa mkono na jeshi, kundi la Udugu wa Kiislamu na washirika wao wametangaza kuwa watafanya maandamano katika maeneo karibu tisa katika mkuu wa Misri,Cairo.

https://p.dw.com/p/19ReB
A child looks out from a car window as supporters of deposed President Mohamed Mursi demonstrate during a slow drive through central London August 17, 2013. Supporters of Mursi fought a gunbattle with security forces in a Cairo mosque on Saturday, while Egypt's army-backed government, facing deepening chaos, considered banning his Muslim Brotherhood group. REUTERS/Luke MacGregor (BRITAIN - Tags: CIVIL UNREST POLITICS RELIGION)
Waandamanaji wanaomuunga mkono Mohammed Mursi 17.8.2013Picha: Reuters

Waandamanaji watakusanyika karibu na mahakama ya katiba kusini mwa mji wa Cairo.

Waungaji mkono wa rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Mursi wanapanga kufanya maandamano mengine mjini Cairo leo Jumapili(18.08.2013), na kuongeza hofu ya umwagikaji zaidi wa damu baada ya mamia ya watu kuuwawa wiki hii.

Police and pro-Egyptian government supporters fight the effect of tear gas outside al-Fath mosque in Cairo August 17, 2013. Gunmen opened fire on security forces from a second floor window in the Fath mosque, where hundreds of Mursi supporters have been taking refuge since protests turned violent on Friday. REUTERS/Muhammad Hamed (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST RELIGION)
mapambano katika msikiti wa al-Fath17.8.2013Picha: Reuters

Kundi la Udugu wa Kiislamu kufutwa kisheria

Maandamano hayo yanakuja wakati serikali inatafakari kulivunjia kabisa kisheria kundi la Udugu wa Kiislamu na waendesha mashtaka wanawahoji wafuasi 250 wa Mursi kuhusiana na mauaji na madai ya ugaidi.

serikali inawashutumu viongozi wa makundi ya Kiislamu kwa kuchochea ghasia na imeahidi kupambana na kile ilichokiita , "nguvu za ugaidi na uharibifu".

Ghasia zilianza siku ya jumatano wakati majeshi ya usalama yalipowaondoa kwa nguvu waandamanaji katika maeneo mawili makubwa ya waandamanaji wanaomuunga mkono rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Mursi mjini Cairo. Kiasi ya watu 750 wameuwawa katika hatua hiyo ya jeshi pamoja na ghasia zilizofuatia nchi nzima.

REFILE - ADDING VERB Army soldiers react inside a room of al-Fath mosque when supporters of deposed Egyptian President Mohamed Mursi exchanged gunfire with security forces inside the mosque in Cairo August 17, 2013. The gunmen opened fire on security forces from a second floor window in the Fath mosque, where hundreds of Mursi supporters have been taking refuge since protests turned violent on Friday. REUTERS/Muhammad Hamed (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST RELIGION MILITARY TPX IMAGES OF THE DAY)
Ndani ya msikiti wa al-Fath mjini Cairo 17.8.2013Picha: Reuters

Hatua ya jeshi kumuondoa madarakani Mursi , Julai 3 mwaka huu , baada ya maandamano ya mamilioni ya Wamisri wakidai ajiuzulu, imewagawa kwa kiasi kikubwa Wamisri , ambalo ni taifa lenye wakaazi wengi miongoni mwa mataifa ya Kiarabu.

Shutuma kali

Ukandamizaji dhidi ya waandamanaji wa makundi ya Kiislamu umesababisha shutuma kali kutoka kwa jumuiya ya kimataifa, hususan kutoka bara la Ulaya na Marekani. Hata hivyo , mataifa ya ghuba yameeleza kuunga kwao mkono watawala wa mpito nchini Misri.

epa03652744 Egyptian Coptic Christians carry the coffins of victims killed in clashes the day before, during the funeral mass at the Abbassiya Cathedral, in Cairo, Egypt, 07 April 2013. According to security officials on 06 April, four Christians and one Muslim were killed and nine others injured in clashes between Muslims and Christians north of Cairo. The violence erupted late 05 April after Coptic Christians spray-painted Christian symbols on a local mosque and an Islamic institution in the working-class area of al-Khusus in the province of Qaliubia. EPA/KHALED ELFIQI
Mazishi katika kanisa la Coptic mjini CairoPicha: picture-alliance/dpa

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema jana jumamosi (17.08.2013) kuwa anashtushwa na maandamano yenye ghasia pamoja na matumizi ya nguvu kupita kiasi ya polisi.

Ban amewataka waandamanaji mitaani na maafisa kuwa na uvumilivu wa hali ya juu na kuelekea haraka katika kupunguza ghasia hizo. Wakati huo huo polisi ya Misri imewaondoa waandamanaji wa Kiislamu kutoka katika msikiti mjini Cairo jana Jumamosi baada ya mapambano ikiwa ni pamoja na kurushia risasi, wakati idadi ya vifo katika siku hizo nne za machafuko ikifikia 750.

Majeshi ya usalama yaliwaondoa waungaji mkono wa rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Mursi kutoka msikiti wa Al-Fath, huku kundi kubwa la watu wenye hasira likijaribu kuwapiga watu hao wakiwaita magaidi.

Mapambano hayo yamekuja wakati serikali ikisema kuwa watu 173 wameuwawa katika muda wa saa 24 zilizopita , na kufikisha idadi ya watu waliouwawa nchi nzima kufikia 750 tangu siku ya Jumatano, wakati polisi walipowaondoa waandamanaji kwa nguvu katika makambi mawili ya watu wanaomuunga mkono Mursi katika mji mkuu.

Bildnummer: 59927292 Datum: 01.07.2013 Copyright: imago/Xinhua United Nations Secretary-General Ban Ki-moon addresses a press conference after attending the opening ceremony of the High-level Segment of United Nations Economic and Social Council (ECOSOC) Substantive Session 2013 in Geneva, Switzerland, July 1, 2013. Ban Ki-moon on Monday called to end the violence in Syria and said that an international conference on Syria was the best chance for reaching a political solution to end the conflicts. (Xinhua/Wang Siwei) (zw) SWITZERLAND-GENEVA-UN-SYRIA PUBLICATIONxNOTxINxCHN people xas x0x 2013 quer premiumd 59927292 Date 01 07 2013 Copyright Imago XINHUA United Nations Secretary General Ban KI Moon addresses a Press Conference After attending The Opening Ceremony of The High Level Segment of United Nations Economic and Social Council ECOSOC Substantive Session 2013 in Geneva Switzerland July 1 2013 Ban KI Moon ON Monday called to End The Violence in Syria and Said Thatcher to International Conference ON Syria what The Best Chance for Reaching a Political Solution to End The conflicts XINHUA Wang Siwei ZW Switzerland Geneva UN Syria PUBLICATIONxNOTxINxCHN Celebrities x0x 2013 horizontal premiumd
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki MoonPicha: imago/Xinhua

Kwingineko nchini Misri baada ya kuchoma moto shule ya watawa wa Franciscan , waislamu waliwatembeza watawa wawili wa kike barabarani kama "wafungwa wa kivita" kabla ya mwanamke mmoja Muislamu kuomba kuwapa hifadhi. Wanawake wengine wawili waliokuwa wakifanyakazi katika shule hiyo walishambuliwa kingono na kutukanwa wakati wakijaribu kupita katika kundi la watu.

Mwandishi: Sekione Kitojo / ape / afpe / dpae

Mhariri : Amina Abubakar