1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uhispania mabingwa wapya dunia

Aboubakary Jumaa Liongo12 Julai 2010

Uhispania wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa kandanda wa dunia kwa mara ya kwanza huko nchini Afrika Kusini, baada ya kuifunga Uholanzi bao 1-0.

https://p.dw.com/p/OGYM
Mabingwa wapya wa dunia Uhispania na kombe laoPicha: AP

Bao hilo lilifungwa na Andreas Iniesta dakika chache kabla ya kumalizika kwa muda wa nyongeza, baada ya timu hizo kutoka suluhu katika muda wa kawaida. Uhispania pia ndiyo mabingwa wa Ulaya

Fußball-Nationalspieler Thomas Müller
Thomas MüllerPicha: picture alliance / dpa

Wakati huo huo mshambuliaji wa Ujerumani Thomas Muller amekuwa mfungaji bora wa michuano hiyo kutokana na mabao matano aliyofunga.Pia Muller ameteuliwa kuwa mchezaji bora kijana katika michuano hiyo.Diego Follan wa Uruguay alichaguliwa kuwa mwanasoka bora.

Kabla ya kuanza kwa pambano hilo la fainali kati ya Uholanzi na Uhispania, Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela aliingia katika uwanja wa Soccer City akiwa kwenye gari la wazi ambapo alishangiliwa sana wakati alipozungushwa kuwasalimia watazamaji.

Mwandishi:Aboubakary Liongo