1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uholanzi yaizuwia Ujerumani

12 Julai 2013

Mabingwa watetezi wa kombe la mataifa ya Ulaya kwa upande wa wanawake Ujerumani imeshikwa shati na Waholanzi mwanzoni mwa michuano hiyo nchini Sweden.Kocha mpya wa Bayern Munich Pep Guardiola aishutumu Barcelona .

https://p.dw.com/p/1971n
Celia Okoyino da Mbabi (l) of Germany fights for the ball with Daphne Koster of the Netherlands during the UEFA Women's EURO 2013 Group B soccer match between Germany and the Netherlands at the Växjö Arena in Vaxjo, Sweden, 11 July 2013. Photo: Carmen Jaspersen/dpa +++(c) dpa - Bildfunk+++
Pambano kati ya wanawake wa Ujerumani na UholanziPicha: picture-alliance/dpa

Mabingwa watetezi Ujerumani walitoka sare ya bila kufungana na Uholanzi siku ya Alhamis katika mchezo wao wa ufunguzi katika kundi B la mashindano ya ubingwa wa mataifa ya Ulaya kwa wanawake nchini Sweden.

German Coach Silvia Neid before the UEFA Women's EURO 2013 Group B soccer match between Germany and the Netherlands at the Växjö Arena in Vaxjo, Sweden, 11 July 2013 on the field. Photo: Carmen Jaspersen/dpa +++(c) dpa - Bildfunk+++
Kocha wa Ujerumani Silvia NeidPicha: picture-alliance/dpa

Katika mchezo mwingine wa kundi B Iceland ilipata bao la dakika za mwisho na kupata point moja muhimu katika mchezo uliotoka sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Norway. Hakuna timu ambayo imeweza kupata ushindi katika fainali hizi za kombe la mataifa ya Ulaya kwa wanawake hadi sasa, baada ya wenyeji Sweden kutoka sare na Denmark na Italia ikatoka sare pia na Finland katika kundi A.

Outside the Växjö Arena before the UEFA Women's EURO 2013 Group B soccer match between Germany and the Netherlands in Vaxjo, Sweden, 11 July 2013. Photo: Carmen Jaspersen/dpa +++(c) dpa - Bildfunk+++
Uwanja unaofanyika mapambano wa Växjö ArenaPicha: picture-alliance/dpa

Pep aishutumu Barca

Kocha mpya wa Bayern Munich Pep Guardiola amezusha kimbunga katika vyombo vya habari nchini Uhispania wiki hii baada ya kuwashutumu waajiri wake wa zamani Barcelona kwa kujaribu kutumia ugonjwa wa kocha Tito Vilanova kumshutumu.

Dzsenifer Marozsan (M) of Germany challenges for the ball with Daphne Koster (r) and Goalkeeper Loes Geurts of Netherlands during the UEFA Women's EURO 2013 Group B soccer match between Germany and the Netherlands at the Växjö Arena in Vaxjo, Sweden, 11 July 2013. Photo: Carmen Jaspersen/dpa +++(c) dpa - Bildfunk+++
Mchezaji wa Ujerumani akilishambulia lango la UholanziPicha: picture-alliance/dpa

kocha huyo mwenye umri wa miaka 42, ambaye ameshinda mataji 14 kati ya mwaka 2008 na 2012 akiwa na Barcelona na akawa na mapumziko ya mwaka mmoja mjini New York kabla ya kujiunga na vigogo wa soka la Ujerumani Bayern Munich , ameweka wazi mpasuko kati yake na rais wa Barca Sandro Rosell pamoja na kikosi chake kizima cha uongozi.

Bayerns Trainer Pep Guardiola sitzt am 11.07.2013 im italienischen Riva bei einer Pressekonferenz. Der Bundesligist bereitet sich vom 04.07.2013 bis 12.07.2013 in einem Trainingslager in Arco auf die Saison 2013-14 vor. Foto: Karl-Josef Hildenbrand/dpa +++(c) dpa - Bildfunk+++
Kocha wa FC Bayern Pep GuardiolaPicha: picture-alliance/dpa

Makamu wa rais wa Barcelona hata hivyo amesema amestushwa aliposikia matamshi ya Guardiola na amekana kuwa klabu hiyo imetoa madai dhidi yake.

Celtic's Victor Wanyama (R) vies for the ball with Dmitri Kombarov (L) of Spartak Moskva during their UEFA Champions League group G football match at the Luzhniki stadium in Moscow on October 2, 2012. AFP PHOTO / YURI KADOBNOV (Photo credit should read YURI KADOBNOV/AFP/GettyImages)
Victor Wanyama kuliaPicha: AFP/Getty Images

Usajili

Klabu ya Serie A nchini Italia ya Napoli imepata saini ya mshambuliaji kutoka Hispania Jose Callejon kutoka klabu ya Real Madrid. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye ametokea katika academi ya soka ya Real ataitumikia klabu hiyo kwa muda wa miaka minne.

Wakenya wameingiwa na shauku kubwa baada ya mchezaji wa tiumu ya taifa ya Kenya Harambee Stars Victor Wanyama kumwaga wino kwa klabu ya Premier League ya Southampton kutoka Celtic ya Scottland kwa kitita cha pauni za Uingereza milioni 12.5. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 amekubali mkataba wa miaka minne.

Shirikisho la soka nchini Kenya lilikuwa la kwanza kumpongeza Wanyama , likisema Wanyama , ambaye alichukua wadhifa wa nahodha wa Harambee Stars kutoka kwa Dennis Oliech Juni mwaka huu, ameendelea kuwa balozi mzuri wa Kenya katika soka kutokana na jinsi anavyofanya mambo yake uwanjani.

Je Rooney atahama ManU

Wayne Rooney anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja baada ya kupata maumivu katika mguu wake wakati wa mazowezi kabla ya mchezo wa kirafiki kati ya Manchester United na Thailand All Stars.

Ronney amerejea nchini Uingereza asubuhi ya Ijumaa, lakini uvumi unasema huenda anaishinikiza klabu hiyo ili imuuze katika klabu nyingine. Uvumi huo unaongezwa na ukweli kwamba Rooney hajisikii vizuri hivi sasa na kikosi cha kocha mpya David Moyes na kocha wa Chelsea ambako anasemekana anataka kuhamia Jose Mourinho amekiri kuwa anampenda sana sana wayne Rooney.

©Marcello Pozzetti ©IPS/Marcello Pozzetti ©IPS/MAXPPP - 06/09/2011 ; LONDON ; UK - Wayne Rooney of England during England vs Wales for the Uefa Eoro2012 Group G qualifiers at the Wembley Stadium in London on 06/09/2011. Picture By Marcello Pozzetti ©IPS Photo Agency:21 Delisle Road London SE28 0JD - Personal mobile: 07973 308 835 . ******************* UK OUT *******************
Wayne RooneyPicha: picture-alliance/dpa

Mourinho hata hivyo amesita kusema iwapo anamatumaini ya kumsajili nyota huyo wa Manchester United.

Kocha wa Afrika kusini Gordon Igesund anaihofia Namibia wakati timu hizo zinakaribia kuumana katika robo fainali ya kombe la Cosafa nchini Zambia leo jioni. Namibia iliishangaza Bafana Bafana mara mbili katika michezo hiyo huko nyuma ya kuwania ubingwa wa mataifa ya kusini mwa Afrika.

Mwandishi: Sekione Kitojo / afpe / ape / rtre

Mhariri: Mohammed Abdul Rahman