1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani Kupata rais mpya

Sekione Kitojo18 Machi 2012

Joachim Gauck , mwenye umri wa miaka 72, mwanaharakati wa zamani kutoka iliyokuwa Ujerumani ya mashariki anatarajiwa kuchaguliwa kuwa rais mpya wa tatu nchini Ujerumani katika muda wa miaka miwili.

https://p.dw.com/p/14MIX
Der ehemalige DDR-Buergerrechtler, fruehere Leiter der Stasi-Unterlagen-Behoerde und Kandidat von SPD und Gruenen bei der Bundespraesidentenwahl 2010, Joachim Gauck, liest am Montag (09.01.12) in der Konzerthalle in Karlsruhe aus seiner Autobiographie "Winter im Sommer - Fruehling im Herbst". Foto: Ronald Wittek/dapd
Mgombea wa wadhifa wa urais Joachim GauckPicha: dapd

Gauck anachaguliwa baada ya kupata kuungwa mkono kutoka katika vyama vya kisiasa nchini humo, lakini mwanathiolojia huyo huenda akawa mshirika mgumu kwa kansela wa Ujerumani Angela Merkel.

Merkel amemkubali Gauck kwa shingo upande kushika wadhifa huo ambao ni wa heshima tu , baada ya mshirika katika serikali yake ya mseto kujiunga na vyama vya upinzani mwezi uliopita kumuunga mkono katika hatua ya kuchukua nafasi ya Christian Wulff, aliyejiuzulu kufuatia kuhusika katika kashfa ya kupata takrima ya fedha.

German Chancellor Angela Merkel attends a debate before a parliamentary vote on a Greek bailout package in the Bundestag, the lower house of parliament, in Berlin , February 27, 2012. Germany's parliament was almost certain to endorse a second Greek bailout on Monday but Chancellor Angela Merkel was torn between domestic pressure to stop throwing good money after bad and global calls to boost Europe's crisis defences. REUTERS/Thomas Peter (GERMANY - Tags: POLITICS BUSINESS)
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel (CDU)Picha: Reuters

Tofauti na Wulff, ambaye ni mbunge wa zamani kutoka chama tawaka cha kansela Merkel cha CDU, Gauck hana mafungamano na chama chochote, Lakini anafahamika kwa kusema kile anachofikiria , kwa hali ambayo ni kama anahubiri, hata katika masuala yenye utata.

ARCHIV - Bundespräsident Christian Wulff nimmt am Sonntag (22.01.2012) im Berliner Ensemble in Berlin an einem «Zeit»-Matinee zum Thema «Deutsche, ihre Identität und ihre Rolle in Europa» teil.Die Staatsanwaltschaft Hannover prüft den gemeinsamen Urlaub von Bundespräsident Christian Wulff mit dem Filmunternehmer David Groenewold im Herbst 2007 auf Sylt. Die Behörde habe davon Mitte Januar aus den Medien erfahren, sagte Oberstaatsanwalt Hans-Jürgen Lendeckel der Nachrichtenagentur dpa am Mittwoch in Hannover. Foto: Wolfgang Kumm dpa/lni (zu dpa 1152 vom 08.02.2012) +++(c) dpa - Bildfunk+++ Copyright: picture alliance / dpa
Rais aliyelazimika kujiuzulu Christian WulffPicha: picture-alliance/dpa

Kwa mujibu wa uchunguzi wa maoni uliofanywa na shirika la Infratest siku ya Jumamosi, asilimia 80 ya Wajerumani wanamuamini Gauck, mchungaji wa zamani wa kanisa la Lutheran na mwanaharakati wa kupigania haki za binadamu. Hata hivyo theluthi mbili wamesema kuwa wanafikiria atakuwa ni rais ambaye vyama vya siasa havitajisikia kuwa katika hali ya utulivu nchini humo.

Nchini Ujerumani, rais anachaguliwa sio na wapiga kura wa kawaida lakini huchaguliwa na baraza maalum lenye wajumbe 620 kutoka bunge la Ujerumani , Bundestag na idadi kama hiyo ya wawakilishi wa majimbo 16 ya Ujerumani .Kuchaguliwa kwa Gauck ni hakika kwasababu anaungwa mkono na vyama vitatu ikiwa ni pamoja na chama tawala cha CDU na kile cha upinzani cha SPD na kijani.

"Tunatarajia wingi mkubwa kwa Gauck" amesema Frank-Walter Steinmeier, kiongozi wa chama cha upinzani cha Social Democratic. Mpinzani wake pekee ni Beate Klarsfeld, mwenye umri wa miaka 73, mwanaharakati anayepambana dhidi ya Wanazi, ambaye ameteuliwa na chama kidogo cha Die Linke.

Bundesaussenminister Frank-Walter Steinmeier (SPD) steht am Donnerstag, 29. Dezember 2005, im Krisenzentrum des Auswaertigen Amtes in Berlin vor einer Karte des Jemen und beantwortet Fragen von Journalisten. Der Politiker aeusserte sich gegenueber Medienvertretern zum Stand der Entfuehrung des ehemaligen Staatssekretaers Juergen Chrobog und dessen Familie im Jemen. (AP Photo/Wolfgang Kumm, pool) ----German Foreign Minister Frank-Walter Steinmeier answers journalists' questions on the kidnapping of former German Foreign Ministery's top official Juergen Chrobog in Yemen as he stands in front of a map of Yemen prior to a meeting of the crisis committee in Berlin Thursday, Dec. 29, 2005. (AP Photo/Wolfgang Kumm, pool)
Mkuu wa chama cha upinzani cha SPD Frank-walter SteinmeierPicha: AP

Kiongozi wa taifa la Ujerumani hana madaraka makubwa ya kiutendaji lakini anatarajiwa kutoa uongozi wa kimaadili , jukumu ambalo Gauck , ambaye ni mtu mashuhuri katika vuguvugu la maandamano ya amani ambayo yamesababisha kuanguka kwa ukuta wa Berlin mwaka 1989, anaonekana kulimudu sana.

Mwandishi : Sekione Kitojo / RTRE

Mhariri : Amina Abubakar.