1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani kupimana ubavu na Italia

Sekione Kitojo
14 Novemba 2016

Ujerumani inakabiliana na Italia kesho Jumanne(15.11.2016)kwa mchezo wa kirafiki ambao utafanyika katika uwanja  wa San Siro, pambano ambalo kwa kawaida hutoa cheche miamba hiyo ya soka  barani Ulaya inapokutana.

https://p.dw.com/p/2SgO4
Fußball Länderspiel San Marino v Deutschland
Mchezaji wa Ujerumani Serge Gnabry akipongezana na Jonas Hector baada ya kufunga baoPicha: picture-alliance/AP Photo/M. Vasini

Ikiwa  bado  inakabana  na  Uhispania  kwa  kuwa  na pointi  sawa  katika  kundi  G, Italia  itarejea  katika  mfumo wake  wa  kawaida  wa  3-5-2  kwa  mchezo  wa  kesho dhid  ya  Ujerunani  baada  ya  kuamua kutumia  mfumo  wa  4-2-4  na kuikandamiza  Liechtenstein  kwa  mabao  4-0  siku  ya Jumamosi.

Hata  hivyo  matumaini  ya  ushindi  kwa  vijana  wa Joachim Loew , ambao  walishinda  mchezo  wa  kirafiki Machi  mwaka  huu  kwa  mabao  4-1  mjini  Munich  kabla ya  kuishinda  Italia  tena  kwa  mikwaju  ya  penalti  katika robo  fainali  ya  Euro  2016  katikati  ya  mwaka  huu , yatakuwa  juu.

Fußball WM-Qualifikationsspiel Italien vs Mazedonien
Ciro Immobile mshambuliaji wa ItaliaPicha: Getty Images

Loew , ambaye  aliweka  rekodi  mpya  ya  kufikisha ushindi  wa  michezo  95  akiwa  na  timu  ya  taifa  ya Ujerumani   wakati  Die Mannschaft  ilipoishindilia  San Marino  kwa  mabao  8-0  siku  ya  Ijumaa, inatarajiwa kutumia  mchezo  huo  kufanya  majaribio  wakati  jicho likiwa  katika  kombe  la  mabara  la  dunia  la Confederation. baada  ya  ushindi  huo ambapo  mchezaji chipukizi Serge Gnabry  alipachika  mabao  matatu, mchezaji  wa  kati  kutoka  Manchester  City Ilkay Gundogan  alikuwa  na  haya  ya  kusema.

"Ni  wazi  kwamba  kwa  sasa  hakuna  kipimo  maalum kwetu. Pamoja  na  hayo  ilikuwa  muhimu  kuweka mwendelezo  uwezo  wa  mchezo  wetu.  Kwa  kupata mabao  mawili  ya  mapema, hali  ilikuwa  nzuri. Haikuwa rahisi  hata  hivyo, dhidi  ya  watu  kumi, ambao  wako katika  ulinzi, hilo  pia  lilikuwa  wazi. Hatimaye  tulishinda kwa  mabao  8-0. Kwa   hiyo  kila  kitu  kiko sawa na  mambo  yanaendelea."

Mchezaji  wa  kati  wa  Juventus  Turin Sami  Khedira   na mchezaji  wa  kati  wa  Arsenal Mesut Ozil  wote watapumzishwa, ikiwa  na  maana  kwamba  huenda mchezaji  wa  Wolfsburg Yannick Gerhart atapewa  nafasi ya  kucheza  kwa  mara  ya  kwanza  katika  kikosi  hicho.

Wakati  mlinda  mlango  wa  kawaida  manuel Neuer  akiwa nje  kutokana  na  homa, Bernd Leno  wa  Bayer Leverkusen  atapewa  wajibu  wa  kuwazuwia washambuliaji  wa  Squadra  Azzuri  wasifanye  kile wanachokifanya  kila  mara  dhidi  ya  Die Mannschaft.

Leo  kikosi  hicho  cha  Die Mannschaft  kilikutana  na kiongozi  wa  kanisa  Katoliki  duniani  Papa  Francis  mjini Vatican  kabla  ya  kuanza  matayarisho  ya  mchezo  huo wa  kirafiki  dhidi  ya  Italia.

Vatikan Papst Franziskus empfängt deutsche Fußball-Nationalmannschaft
Papa Francis akipokea kitambaa kilichochorwa na watoto wanaohudumiwa na wakfu wa mlinda mlango wa Die Mannschaft Manuel NeuerPicha: picture-alliance/Catholic Press Photo/IPA

Thomas Mueller  na  Mats Hummels  wa  Bayern  Munich walimkabidhi  Papa  Francis  jezi  ya  Ujerumani  iliyotiwa saini  na  wachezaji  wa  kikosi  hicho  na  kitambaa kilichochorwa  na  watoto  kutokana  na   wakfu ulioanzishwa  na  mlinda  mlango  wa  timu  hiyo  manuel Neuer.

Pope  ambaye  ni  shabiki  mkubwa  wa  kandanda ambaye  timu  ya  nyumbani  kwao  Argentina  ilipoteza mchezo  wa  fainali  ya  kombe  la  dunia  mwaka  2014 dhidi  ya  Ujerumani , alisifu  ujasiri  wa  timu  ya  taifa  ya Ujerumani.

"Niliwahi mara  nyingi kusikia  kwamba  ushindi  wenu  ni ushindi  wa  timu," alisema  papa  Francis  akitambua kwamba  timu  hiyo  inafahamika  kama  Die Mannschaft, yaani  kikosi.

 

Mwandishi:  Sekione  Kitojo

Mhariri: Yusuf  Samu