1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yaifungisha virago Argentina

4 Julai 2010

Ujerumani itakumbana na mabingwa wa Ulaya, Spain katika nusu fainali ya Kombe la Dunia Jumatano ijayo, baada ya kuwafungisha virago Argentine katika mchezo wa kusisimua uwanjani Green Point mjini Cape Town.

https://p.dw.com/p/OAGX
Members of the Germany team pose for pictures prior to the World Cup quarterfinal soccer match between Argentina and Germany at the Green Point stadium in Cape Town, South Africa, Saturday, July 3, 2010. Top row, from left, Manuel Neuer, Sami Khedira, Arne Friedrich, Per Mertesacker, Jerome Boateng and Miroslav Klose. Bottom row, from left, Philipp Lahm, Mesut Oezil, Lukas Podolski, Thomas Mueller and Bastian Schweinsteiger. (AP Photo/Roberto Candia)
Timu ya Ujerumani kabla ya kupambana na Argentine katika robo fainali ya Kombe la Dunia, uwanjani Green Point mjini Cape Town, Afrika Kusini.Picha: AP

Ujerumani ilirudia historia, kwa kuwashinda Argentina katika robo fainali ya Kombe la Dunia kwa mara ya pili mfulilizo. Mabao manne ya Ujerumani yalitosha kumpokonya Maradona uwezekano wa kuwa mtu wa tatu katika historia kushinda taji la kombe la dunia kama mchezaji na kocha.

Germany's Thomas Mueller, second left, scores a goal on a header past Argentina's Sergio Romero, left, during the World Cup quarterfinal soccer match between Argentina and Germany at the Green Point stadium in Cape Town, South Africa, Saturday, July 3, 2010. (AP Photo/Michael Sohn)
Thomas Mueller wa Ujerumani (pili kutoka kushoto) akilifuma lango la Argentina.Picha: AP

Thomas Mueller alifungua awamu ya mabao ya Ujerumani na baadae Miroslav Klose akafunga mabao mawili katika kipindi cha pili.

Klose sasa amefunga mabao 14 katika Kombe la Dunia. Ikiwa atafunga bao lingine moja basi atafikia rekodi ya mabao 15 iliyowekwa na Ronaldo wa Brazil.

Na katika mechi nyingine iliyochezwa hiyo jana, David Villa ndie aliyeiokoa Spain katika robo fainali ya pili, dhidi ya Paraguay.

Spain's David Villa, right, controls the ball ahead of Paraguay's Paulo Da Silva, left, during the World Cup quarterfinal soccer match between Paraguay and Spain at Ellis Park Stadium in Johannesburg, South Africa, Saturday, July 3, 2010. (AP Photo/Rebecca Blackwell)
David Villa wa Spain(kulia) akiudhibiti mpira kabla ya Paulo Da Silva wa Paraguay.Picha: AP

Bao la Villa katika dakika ya 83 liliikatia Spain tiketi ya nusu fainali ya dimba la kombe la dunia kwa mara ya kwanza kabisa. Timu zote mbili zilipata mikwaju ya penalti lakini hazikuweza kufunga. Mechi ya Spain na Ujerumani itakuwa marudiano ya fainali ya Kombe la Mabingwa wa Ulaya- Spain ndio ilifanikiwa kuondoka na ushindi.

Mwandishi: Munira Muhammad/APE