1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yailaumu Marekani

12 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CamT

BALI.Waziri wa Mazingira wa Ujerumani Sigmar Gabriel ameilaumu Marekani kwa msimamo inaouchukua katika suala la mabadiliko ya hali ya hewa.

Akizungumza katika mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya hali ya hewa huko Bali Indonesia, Sigmar amesema kuwa Marekani imekuwa kikwazo katika harakati za kimataifa kufikia mkataba mpya wa hali ya hewa.

Mapema Katibu Mkuu wa Mataifa Ban Ki moon alitoa wito kwa nchi zote kukubaliana na mkataba wa kupambana na ongezeko la ujoto duniani ifikapo mwaka 2009.

Mawaziri wa Mazingira na wakuu kadhaa wa serikali watatumia siku tatu za mwisho za mkutano huo kujaribu kuweka muundo wa kupambana na mabadiliko ya hali hewa kabla ya mwaka 2012 wakati mkataba wa Kyoto utakapomalizika.