1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yaingia robo fainali UEFA 2012

18 Juni 2012

Katika kinyang'anyiro cha mashindano UEFA EURO 2012, Ujerumani na Ureno za kundi B zimefanikiwa kuingia robo fainali ya mashindano hayo yanayofanyika Poland na Ukraine, matokeo yaliyopokewa vyema na washabiki.

https://p.dw.com/p/15H2R
Wachezaji wa Ujerumani wakishangiria ushindi wao wa 2-1 dhidi ya Denmark.
Wachezaji wa Ujerumani wakishangiria ushindi wao wa 2-1 dhidi ya Denmark.Picha: Reuters

Ujerumani imetinga hatua hiyo baada ya kuiadhibu Denmark bao 2-1 kwenye mchezo wa jana, huku Ureno nayo ikiitoa nje ya mashindano Uholanzi kwa kipigo cha namna hiyo cha bao 2-1. Ujerumani ndiyo kinara wa kundi B kwa pointi 9, ikifuatiwa na Uholanzi yenye pointi 6. Kwa matokeo hayo, sasa Ujerumani itakwaana na Ugiriki kwenye mchezo wa robo fainali. Ugiriki ndiyo iliyoifanya Urusi ifunge virago vyake Jumamosi iliyopita baada ya kuichapa bao 1-0.

Mwandishi: Stumai George
Mhariri: Oummilkheir Hamidou