1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yainusuru Benki ya Mikopo ya Nyumba

md6 Oktoba 2008

Serikali ya Ujerumani, Benki Kuu, pamoja na wadau wengine wa sekta ya fedha wamekubaliana na kuongeza kiwango cha fedha ili kuinusuru benki ya mikopo ya nyumba ya Ujerumani Hypo Real Estate inayokabiliwa na hali mbaya

https://p.dw.com/p/FUZY
Kansela Angela Merkel akiwa pamoja na Waziri wa Fedha Peer Steinbrück katika mkutano na waandishi wa habari mjini BerlinPicha: picture-alliance /dpa

Makubaliano hayo mapya ya kiasi cha euro billioni 50 ya kuipatia benki hiyo ambayo ni ya pili kwa ukubwa hapa Ujerumani, yalifuatia kushindwa mpango wa awali wa euro billioni 35 zilizokuwa zitolewe na taasisi nyingine za fedha.


Mapema Kansela wa Ujerumani Angela Merkel alitangaza mipango ya kuhakikisha usalama wa fedha za watu binafsi katika mabenki kufuatia mzozo huo wa kibenki.


Akizungumza na waandishi wa habari akiwa pamoja na Waziri wa Fedha wa Ujerumani Peer Steinbrueck, mjini Berlin Kansela Merkel aliahidi kudhibiti msukosuko huo katika mfumo wa fedha na kuongeza kuwa ana daiwa na walipa kodi wa Ujerumani kuchukua hatua hatua mujaribu.