1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yazindua kikosi chake cha mwanzo

23 Mei 2014

Kocha wa Ujerumani Joachim Löw ameitaja orodha yake ya wachezaji 30 lakini watakaoiwakilisha nchi katika Kombe la Dunia nchini Brazil, akawashangaza wengi kwa kuwatema nje wachezaji wenye ujuzi kama vile Mario Gomez.

https://p.dw.com/p/1BxFG
Joachim Loew Löw Bundestrainer FIFA Weltmeisterschaft 8.5.2014
Picha: Alex Grimm/Bongarts/Getty Image

Aliwajumuisha kikosini wachezaji wasiojulikana sana, kama vile beki wa Genoa Shkrodan Mustafi, beki wa Borussia Dortmund Erik Durmm, kiungo mshambuliaji wa Augsburg Andre Hahn, mshambuliaji wa Hoffenheim Kevin Volland na viungo wa Schalke wenye umri wa miaka 19 Max Meyer na Leon Goretzka. Wote hao hawajahi kuichezea timu ya taifa lakini Löw ameutetea uamuzi wake huo

Löw amesema kuwa hana wasiwasi yoyote kuhusiana na kila mmoja wa wachezaji waliochaguliwa. Gomez ambaye ana magoli 25 katika mechi 59 alizoichezea Ujerumani, amekosa nafasi kutokana na jeraha lagoti lake la kushoto, baada ya msimu uliokumbwa na majeraha katika klabu ya Fiorentina nchini Italia.

Pia hakukuwa na nafasi ya mlinda lango wa Borussia Moenchengladbach Marc-Andre ter Stegen wala kipa wa zamani nambari moja wa Ujerumani Rene Adler. Mlinda lango wa Borussia Roman Weidenfeller na mwenzake wa Hannover Ron-Robert Zieler wamechaguliwa pamoja na kipa nambari moja wa sasa Manuel Neuer wa Bayern Munich.

Mario Gomez ametatizika sana na majeraha msimu huu tangu ahamie ligi kuu ya soka nchini Italia
Mshambuliaji Mario Gomez ametatizika sana na majeraha msimu huu tangu ahamie ligi kuu ya soka nchini ItaliaPicha: Alexander Hassenstein/Bongarts/Getty Images

Löw amemwita kikosini Sami Khedira kiungo wa Real Madrid ambaye hajaichezea klabu hiyo tangu mwezi Novemba mwaka jana baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti. Bayern imechangia wachezaji saba, Borussia Dortmund imewatoa wachezaji sita wakati Arsenal ya Uingereza ikiwatoa wachezaji watatu.

Kocha huyo ana hadi Mei 13 kuwasilisha kwa FIFA orodha yake ya mwisho isiyozidi wachezaji 30, huku muda wa mwisho wa kuwasilisha kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 ukiwa Juni 2. Na kutokana na fainali ya kombe la Shirikisho la Soka la Ujerumani – DFB kati ya Bayern Munich na Borussia Dortmumd, itakayochezwa mjini Berlin Mei 17, Löw amekitaja kikosi tofauti cha wachezaji 18 kitakachocheza mchuano wa kirafiki Jumanne wiki ijayo dhidi ya Poland mjini Hamburg.

Kikosi cha mwanzo

Walinda lango: Manuel Neuer, Roman Weidenfeller, Ron–Robert Zieler

Defenders: Jerome Boateng, Erik Durm, Kevin Grosskreutz, Benedikt Höwedes, Mats Hummels, Marcell Jansen, Philipp Lahm, Per Mertesacker, Shkodran Mustafi, Marcel Schmelzer

Viungo: Lars Bender, Julian Draxler, Matthias Ginter, Leon Goretzka, Mario Götze, Andre Hahn, Sami Khedira, Toni Kroos, Max Meyer, Thomas Müller, Mesut Özil, Lukas Podolski, Marco Reus, Andre Schürrle, Bastian Schweinsteiger

Washambuliaji: Miroslav Klose, Kevin Volland

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA
Mhariri: Yusuf Saumu