1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ulaya yajitetea mkutano wa G20

19 Juni 2012

Mwanzoni mwa mkutano wa kundi la mataifa yaliyoendelea kiviwanda na yale yanayoinukia kiuchumi G20 nchini Mexico , suala la mzozo wa madeni katika mataifa yanayotumia sarafu ya euro lilikuwa mada kuu.

https://p.dw.com/p/15Hba
Leaders of the G20 nations (First row L-R), France's President Francois Hollande, Argentina's President Cristina Fernandez, Indonesia's President Susilo Bambang Yudhoyono, U.S. President Barack Obama, China's President Hu Jintao, Mexico's President Felipe Calderon, South Korea's President Lee Myung-bak, South Africa's President Jacob Zuma, Brazil's President Dilma Rousseff, Russia's President Vladimir Putin, (Middle row L-R), European Commission's President Jose Manuel Barroso, Italy's Prime Minister Mario Monti, Turkey's Prime Minister Tayyip Erdogan, Australia's Prime Minister Julia Gillard, Germany's Chancellor Angela Merkel, India's Prime Minister Manmohan Singh, British Prime Minister David Cameron, Canada's Prime Minister Stephen Harper, Japan's Prime Minister Yoshihiko Noda, European Council President Herman Van Rompuy, Saudi Arabia's Finance Minister Ibrahim Alassaf. (Back row L-R), Bank of Canada Governor Mark Carney, OECD Secretary General Jose Angel Gurria, World Bank's President Robert Zoellick, FAO Director-General Jose Graziano da Silva, Spain's Prime Minister Mariano Rajoy, Cambodia's Prime Minister Hun Sen, Colombia's President Juan Manuel Santos, Chile's President Sebastian Pinera, Benin's President Boni Yayi, Ethiopia's Prime Minister Meles Zenawi, United Nations Secretary-General Ban Ki-moon, General-Director of the international Labour Organization Juan Somavia, IMF's Managing Director Christine Lagarde and WTO Director General Pascal Lamy pose for the family picture in Los Cabos June 18, 2012. G20 leaders will kick off two days of meetings in the Pacific resort of Los Cabos on Monday REUTERS/Edgard Garrido (MEXICO - Tags: POLITICS BUSINESS)
Mkutano wa kundi la G20 mjini Los Cabos MexikoPicha: Reuters

Mataifa ya Ulaya yanajitetea kuwa hayahusiki na hali ya sasa ya kudorora kwa uchumi wa dunia.

Viongozi wa mataifa yenye uchumi mkubwa duniani wanataka kujiweka katika hali kwamba wako pamoja nyuma ya juhudi za kuimarisha ukuaji wa uchumi wa dunia pamoja na kutengeneza nafasi za ajira ili kuweza kuufanyia ukarabati uchumi wa dunia ulio tete, na ambao umegubikwa na hofu juu ya mzozo wa kifedha wa mataifa ya Ulaya. Hii ni kwa mujibu wa rasimu ya taarifa ambayo itawasilishwa mwishoni mwa mkutano huo wa kila mwaka wa kundi la G20.

Shutuma dhidi ya Ulaya

Lakini rais wa halmashauri ya umoja wa Ulaya Manuel Barroso jana Jumatatu (18.06) alikanusha vikali kuwa mataifa ya umoja wa sarafu ya euro yanahusika katika kuuporomoa uchumi wa dunia na kwamba mataifa hayo yamechukua muda mrefu kuweza kuchukua hatua za kupambana na hali hiyo.

European Commission President Jose Manuel Barroso addresses the media before the G20 Summit in Los Cabos June 18, 2012. G20 leaders will kick off two days of meetings in the Pacific resort of Los Cabos on Monday. REUTERS/Henry Romero (MEXICO - Tags: POLITICS)
Rais wa halmashauri ya umoja wa Ulaya Manuel BarrosoPicha: Reuters

"Si wanachama wote wa kundi la G20 wanatekeleza demokrasia. Lakini sisi tunatekeleza Demokrasia. Na tunachukua maamuzi yetu kidemokrasia. Baadhi ya nyakati hii ina maana ya kuchukua muda mrefu. Kwa kuwa huu ni muungano wa mataifa 27 ya kidemokrasia, na tunahitaji kutafuta muafaka wa pamoja. Lakini hatukuja hapa kupewa somo kuhusu demokrasia ama jinsi gani ya kuendesha uchumi wetu".

Hakuna hakika , hata hivyo , iwapo maneno ya kutoa uhakika ya viongozi wa kundi la mataifa ya G20 yatatuliza masoko , ambayo mtazamo wake kuhusu jinsi serikali zilivyochukua hatua kupambana na mzozo huu wa madeni , ulionekana kuwa unayasukuma mataifa ya Ulaya karibu na maafa makubwa kila siku. Hapo jana, muda mfupi baada ya uchaguzi nchini Ugiriki hofu ilitulia kuwa nchi hiyo inaweza kujitoa katika sarafu ya euro, na pia hofu kuwa Uhispania iliufikisha uwezo wa kukopa wa uchumi wa nchi hiyo karibu na kiwango cha kuhitaji mpango wa kuiokoa.

Taarifa ya viongozi wa kundi la mataifa ya G20 ni pamoja na lugha ambayo inaonekana kulenga katika kupunguza mzozo wa Uhispania kwa kuwahakikishia wawekezaji kuwa hazina ya Uhispania haitaishia kutumia gharama za mkopo wa euro bilioni 100 za kuyanusuru mabenki ya nchi hiyo uliotangazwa mwezi huu. Hofu kuwa jukumu la kulipa fedha hizo litaiangukia serikali imesaidia kupandisha gharama za kukopa nchini Uhispania kuwa juu ya kiwango cha asilimia 7.

Umuhimu wa kuchochea ajira

Pia taarifa hiyo inaliweka kundi la G20 katika upande wa wale ambao walikuwa wanadai kuwepo mtazamo wa kuunda nafasi za ajira, ikiwa ni pamoja na kupitia matumizi ya serikali, badala ya kubana matumizi ya bajeti pamoja na kupunguza matumizi ya serikali, hali ambayo inahimizwa zaidi na kansela wa Ujerumani Angela Merkel.

Kansela Angela Merkel anataka kutoka katika mkutano huo wa Los Cabos mpango maalum wa utendaji, ambao utachochea ukuaji wa uchumi.

U.S. President Barack Obama meets with German Chancellor Angela Merkel at the G20 Summit in Cannes, Thursday, Nov. 3, 2011. European leaders' long-delayed admission that a break-up of their cherished common currency was a distinct possibility is overshadowing a two-day meeting of the world's largest and fastest growing economies beginning Thursday in this Cote d'Azur resort. (Foto:Charles Dharapak/AP/dapd)
Angela Merkel (kushoto) na rais Barack Obama wa MarekaniPicha: dapd

"Hapa kila bara linapaswa kutoa mchango wake ambapo hadi sasa kama mataifa ya Ulaya tumetakiwa kufanya. Tutachukua msimamo wa pamoja , kwamba matatizo tuliyonayo katika kanda ya euro, ambayo ni pamoja na matatizo ya ukuaji wa uchumi , tutapambana nayo , kwa kufanya mageuzi ya kiuchumi, kubana matumizi katika bajeti, na pia kuchochea ukuaji wa uchumi".

Rais Barack Obama wa Marekani amejaribu kutoa uhakikisho kuwa mataifa ya Ulaya yako karibu na kuchukua hatua sahihi kupambana na mzozo wa kifedha ambao utatuliza masoko na kuyaweka matatizo ya bara hilo mbali na kuuharibu uchumi wa dunia.

Mwandishi : Bergmann, Christina / ZR/ ape / Sekione Kitojo

Mhariri : Mohammed Abdul Rahman